• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

MKUU WA WILAYA AHIMIZA AKINA BABA KUJIHUSISHA KATIKA MALEZI YA WATOTO.

Imewekwa: March 10th, 2025

Mkuu wa wilaya ya Kongwa Mheshimiwa Mayeka Simon Mayeka amewahimiza akina baba kubeba na kulea watoto wao kwani malezi ni ya pande zote mbili na kitendo hicho hakiondoi maana na thamani ya baba bali kinaongeza thamani ya baba katika familia.

Mhe. Mayeka ameyasema hayo jana alipokuwa katika maadhimisho ya siku ya Afya na lishe yaliyofanyika katika Kata ya Sagara Kijiji cha Msingisa na kuhudhuriwa na wananchi, wataalam pamoja na mashirika wadau wa lishe ambapo mhe. Mayeka amebainisha kuwa ulinzi wa familia huanza na chakula Pamoja na malezi bora, lakini wanaume wengi wamekuwa wakikwepa kulea watoto wakidhani kwamba kulea ni jukumu la mama peke yake.

Aidha DC. Mayeka ameongeza kuwa suala la lishe ni suala muhimu sana kwani husaidia kujenga kinga ya mwili hivyo swala hilo halipaswi kuchukuliwa kirahisi kwani linaweza kupelekea Serikali kupata mzigo mkubwa kununua madawa kwaajili ya kutibu maradhi ambayo mengi husababishwa na ukosefu wa lishe bora.

Licha ya kuhimiza umuhimu wa siku ya Afya na lishe ya kijiji kufanyika mara kwa mara katika Kila Kijiji lakini pia Mhe. Mayeka amehimiza wazazi kuwapatia watoto muda wa kucheza, kupumzika na kuhakikisha wanazingatia lishe bora mara wanapofikisha miezi sita tangu kuzaliwa.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Omary Nkullo amesisiza malezi ya watoto na amewapongeza wananchi wa Kijiji cha Msingisa kwa mabadiliko makubwa katika elimu, yaliyochangiwa na hatua ya wanakijiji kuajiri walimu wa kujitolea kufundisha watoto wao na kuwataka kuongeza juhudi hiyo katika suala la utekelezaji wa shughuli za Afya na lishe kijijini.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za afya na lishe za Halmashauri, Afisa lishe wilaya ya Kongwa, Bi Mary Haule amesema kuwa takwimu zinaonyesha kuwa watu 75,895 ni watoto chini ya miaka mitano ambapo 31% ya watoto walio chini ya miaka mitano wamedumaa sawa na watoto 23,537. Ameongeza pia kuwa 14% ya watoto chini ya miaka 15 wana uzito pungufu sawa na watoto 10,625 na katika kipindi cha mwaka 2024 watoto 149 walitibiwa utapiamlo mkali.

Aidha, Bi Haule amesema kuwa Halmashauri inaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutekeleza afua za lishe  kwa kutoa elimu ya lishe kwa wananchi kuzingatia mtindo bora wa lishe kwa kuzingatia makundi sita ya vyakula , kuhimiza umuhimu wa kuepuka mtindo bwete Kwa kufanya mazoezi, kuhimiza  mbinu bora za kilimo na utunzaji mazao, kutoa huduma za malezi ya Watoto, kupeleka watoto shule na kuwapatia lishe za unga wenye virutubisho.

 Vilevile Bi Haule amezitaja changamoto zinazokwamisha utekelezaji wa masuala ya lishe kuwa ni ushiriki duni wa wanaume katika shughuli za afya na lishe, wajawazito kuchelewa kuanza kliniki chini ya wiki 12, idadi ndogo ya wanafunzi wanakula shuleni kutokana na wazazi kutokuchangia chakula, idadi ndogo ya mashine zilizofungwa kifaa cha kuongeza virutubishi Pamoja na ukosefu wa fedha kwaajili ya kuendeshea siku ya afya na lishe kijijini.

Katika maadhimisho hayo huduma mbalimbali zilitolewa zikiwemo huduma za upimaji virusi vya ukimwi, uchunguzi wa Magonjwa yasiyoambukiza kama kisukari na shinikizo la damu, huduma za lishe kwa watoto chini ya miaka mitano, kilimo na usalama wa chakula, elimu ya unawaji wa mikono na elimu ya mapishi ya vyakula mchanganyiko kwa watoto, wajawazito na wanaonyonyesha ili kusaidia kuleta nguvu na kukuwa kirahisi ambapo maadhimisho hayo hufanyika kila baada ya miezi mitatu.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.