• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

MKUU WA WILAYA YA KONGWA AFUNGUA MAFUNZO KWA WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI.

Imewekwa: December 23rd, 2024

Baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa uliopelekea kupatikana kwa viongozi ikiwemo wenyeviti wa vijiji, wenyeviti wa vitongoji, wajumbe wa halmashauri za vijiji mchanganyiko Pamoja na makundi maalimu. Viongozi walioshinda wamepata fursa ya kupatiwa semina ya mafunzo iliyokuwa na mada mbalimbali ili kuwawezesha kufanya majukumu yao kwa ufasaha.


Mgeni rasmi wa semina ya mafunzo hayo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka S. Mayeka akifungua semina za mafunzo hayo kwanza amewapongeza viongozi waliochaguliwa ili kuwatumikia wananchi na kuwasihi kuwa ushirikiano wao ni muhimu ili wananchi wapatiwe huduma muhimu kwa wakati na kero zao zitatuliwe kwa muda mfupi sana.

Mhe. Mayeka pia amewaeleza viongozi hao kuwa wao ni kiunganishi muhimu cha serikali na wananchi kwani wao ndio wako karibu sana na wananchi na wanajua wanayoyapitia wananchi kwa ukaribu sana na utatuzi wa maswala mbalimbali unaanza nao.

Aidha mhe. Mayeka amewasihi viongozi hao kufata taratibu zote za uongozi na maswala watakayofundishwa na wasijiingize kwenye matendo maovu yatakayochafua uongozi wao Pamoja na vyama vyao vya siasa ambavyo vimewaamini na kuwapa dhamana ya kutekeleza ilani ya vyama husika.

Akiongea wakati akimkaribisha mgeni rasmi, mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Omar Nkullo amewashukuru viongozi hao kujitokeza kwa wingi na umoja wao katika mafunzo hayo na kuwasisitiza kuwa umoja huo ndio utakaofanikisha maswala mengi ya kimaendeleo katika maeneo yao ya uongozi.


Baadhi ya mada zilizotolewa kwa viongozi katika semina ya mafunzo ni Pamoja na Sheria za Uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa zitakazokuwa ni muongozo muhimu ili kusaidia viongozi kutekeleza shughuli zao za kila siku.

Mada nyingine ni Pamoja na Muundo, Majukumu na Madaraka ya Vijiji na Vitongoji Pamoja na Uongozi na Utawala bora, ambayo ni mambo muhimu viongozi kuelewa wakati wanapoelekea kutekeleza majukumu yao ya uongozi.

 Viongozi pia wamefunzwa kuhusu uendeshaji wa Vikao na Mikutano katika Ngazi za Vijiji na Vitongoji sababu elimu ya kuendesha vikao ni nguzo muhimu itakayowasaidia kuitisha vikao vinavyojadili ajenda tofauti tofauti ikiwemo ajenda za maendeleo ya vijiji na vitongoji, pia viongozi wamefunzwa kuhusu Uibuaji, Upangaji na Usimamizi wa Miradi Shirikishi ya Kijamii Pamoja na usimamizi na Udhibiti wa Fedha katika Mamlaka za Serkali za Mitaa.


Aidha mada nyingine muhimu zilizowasilishwa kwa viongozi ni Pamoja na Usimamizi wa Ununuzi Pamoja na Usimamizi wa Aridhi na Udhibiti wa Uendelezaji Vijiji.

Viongozi waliopatiwa mafunzo wameahidi kuyatumia vizuri mafunzo hayo ili kuongeza ufanisi katika majukumu yao ya kila siku katika nyadhfa zao kwa madhumuni mapana ya kuwaletea wananchi maendeleo na kutatua changamoto zitakazojitokeza katika maeneo yao ya uongozi

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.