• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

NATURE TANZANIA WAKABIDHI MBUZI 25 KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA MANUNGU NA MORISHENI.

Imewekwa: February 24th, 2025

Shirika la Nature Tanzania linalotekeleza Mradi wa kupunguza mauaji ya ndege aina ya Korongo weupe katika wilaya ya Kongwa na Mpwapwa limegawa mbuzi 25 kwa vikundi viwili vinavyotoka katika Kijiji cha Manungu na Morisheni katika Wilaya ya Kongwa. Huu ni muendelezo wa mradi wake wa kupunguza mauaji ya ndege hao ambapo tathmini imeonyesha kuwa kati ya ndege 500 hadi 1000 huuwawa kila mwaka katika msimu wa masika.

Licha ya kutoa mbuzi pia Nature Tanzania imeendelea kutoa elimu kwa umma juu ya umuhimu wa uhifadhi wa mazingira na ndege kwani ndege hawa husaidia kula wadudu waharibifu wa mashambani kama vile panzi na viwavijeshi.


Meneja wa Mradi kutoka Nature Tanzania Bi. Neema Mwaja, ameeleza katika risala kuwa shirika pia limefanikiwa kutoa elimu ya ufugaji nyuki kwa wanufaika 60 kwa kushirikiana na TFS ambapo wamegawa mizinga 30 ya kisasa katika vijiji mbalimbali wilayani Kongwa ikiwemo Mlanga, Morisheni Manungu na pia shirika limegawa vifaa vya kuvunia asali ikiwemo mavazi, viatu, mashine ya kuchakata na kuchuja asali, ili kuongeza mnyororo wa thamani kwa wanufaika kwa dhumuni la kukuza Uchumi wao.

Akizungumza kabla ya kushiriki zoezi la kukabidhi mbuzi hao, mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka akiongea na wananchi amesisitiza ufugaji wenye tija na kueleza kuwa kutegemea kilimo vipindi ambavyo mazao hayajafanya vizuri ni hatari kwani chakula kinapokosekana, watu huingia katika uwindaji holela ikiwemo uwindaji wa ndege hao ili kusudi wapate vitoweo.

Mhe. Mayeka ametolea mfano nchi ya Sudan ambayo jamii kubwa ni wafugaji na kueleza kuwa Kongwa ikijikita katika ufugaji wenye tija, basi inawezakuuza mifugo na kulilisha jiji la Dodoma na kufanya Kongwa kuwa kitovu cha biashara ya Mifugo na kuongeza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatoa chanjo kwa wafugaji ili kupambana na magonjwa ya mifugo kwa dhumuni la kuwezesha wafugaji kunufaika na biashara hiyo sababu chanjo zimepunguza magonjwa ya mifugo kwa kiasi kikubwa sana.

Akiongea kwa niaba ya wanakikundi walionufaika na mradi, mwenyekiti wa kikundi kutoka Kijiji cha Manungu ametoa shukrani zake za dhati kwa shirika la Nature Tanzania na kuahidi kuwa mbuzi hao watasimamiwa kwa umakini ili wazaliane na kukwamua Uchumi wa familia zao na jamii kwa ujumla. Ameongeza kuwa usimamizi mzuri wa mifugo hiyo utafanya jamii iwe na chakula cha kutosha, fedha zitokanazo na biashara ya mifugo, maendeleo ambayo yataiondoa jamii katika uwindaji wa ndege aina ya Korongo weupe kwa ajili ya kitoweo.

Mradi huu unakuja baada ya utafiti kuonyesha kuwa ndege hawa huuliwa kwa sumu na huuzwa kati ya shilingi 2500- 5000 hivyo kufanya Nature Tanzania kushiriiana na NABU international Foundation kuanzisha mradi wa kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kuwatafutia njia mbadala za kuwapatia kipato ikiwemo ufugaji wa nyuki, ufugaji wa mbuzi na ufugaji wa kuku pamoja na kutoa elimu juu ya uhifadhi ndege vijijini na mashuleni ili kupunguza mauaji ya ndege hao.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.