• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

POLISI KATA PAMOJA NA WATENDAJI KATA WAASWA KUISHI KATIKA KATA ZAO.

Imewekwa: February 21st, 2025

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma SA CP George Katabazi amewataka maafisa Polisi wa Kata Wilayani Kongwa kuishi ndani ya Kata wanazozisimamia ili kusaidia kubaini changamoto za raia wanaowasimamia

Kamanda Katabazi ameyasema hayo katika ziara yake ya kikazi alipotembelea Wilaya ya Kongwa ili kuongea na maafisa wa Polisi na Watendaji Kata juu ya kudumisha ushirikiano baina yao katika kuleta amani na utulivu wa maeneo wanayoyaongoza ambapo sambambsa na hilo ametoa wiki mbili kuhakikisha kila Polisi kata anahamia katika Kata yake.


Aidha Kamanda Katabazi amebainisha kuwa usalama na maendeleo ni vitu vinavyoenda pamoja ili kuvidumisha ni muhimu Polisi Kata, wakaguzi na Watendaji wa Kata kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja kwa kuzingatia mipaka, kanuni, taratibu na sheria zilizopo.

Vilevile Kamanda Katabazi amesisitiza maafisa wa Polisi kuzingatia maadili ya kazi zao na kuacha kujihusisha na vitendo vya uhalifu kama kula rushwa, kuacha kutumia vilevi na kuwaasa kufanya tathmini kama Kata wanazosimamia zina uhalifu ili wapeleke taarifa ya maadhimio ya utekelezaji sehemu husika.


Nae Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mheshimiwa Mayeka Simon Mayeka ametoa rai kwa maafisa Polisi Kata ambao bado Kata zao zina taarifa za ulimaji bangi kujitathmini kwani swala hilo linachafua Kata hizo na utendaji kazi wao. Pia Mhe. Mayeka amegusia suala la kuwaweka watu vizuizini bila sababu kuachwa mara moja ili utulivu uliopo ndani ya Wilaya ya Kongwa uendelee.

Sambamba na hayo Mhe Mayeka ameomba Polisi Kata kupatiwa usafiri utakaowasaidia kufika kirahisi katika maeneo wanayosimamia kwani wanafanya kazi katika mazingira magumu na kugusia kuwa kuna baadhi ya Kata zina Vijiji zaidi ya vitano hivyo inakuwa vigumu kiongozi wa kata kuvifikia Vijiji vyote kwa urahisi.


Hata hivyo Mhe Mayeka amevisihi vyombo vya dola vilivyopo Wilayani Kongwa ikiwemo jeshi la Polisi na jeshi la Wananchi kuacha migogogoro isiyokuwa na maana kwani wote wanategemeana katika kuleta na kudumisha amani katika jamii.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mheshimiwa White Zuberi ameomba jeshi la Polisi kudhibiti wizi wa mifugo ili kunusuru uchumi wa wananchi wanaojihusisha na ufugaji na kukomesha matumizi ya dawa za kulevya na pombe kali ya gongo yanayoendelea ndani ya Wilaya ya Kongwa.



Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.