• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Serikali yajipanga Kutatua Kero za Umeme, Maegesho ya magari na Migogoro ya Ardhi kwa Wakazi wa Kibaigwa Wilaya ya Kongwa.

Imewekwa: July 8th, 2021

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejipanga kutatua kero zinazowakabili kwa muda mrefu Wakazi wa eneo la Kibaigwa wilaya ya Kongwa.

 Miongoni mwa Kero hizo  ni Tatizo la umeme usiokidhi mahitaji, miundombinu ya barabara, migogoro ya Ardhi na huduma za jamii.. 

Akizungumza na Wananchi katika eneo la Kibaigwa Julai 7, 2021,  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, aliahidi kuwa serikali kupitia mamlaka zake itashughulikia kero mbalimbali zinazowakabili wananchi katika eneo hilo.

Katika hotuba yake Mhe. Rais Aliwaasa Wananchi kuchukua Tahadhari dhidi ya Janga la ‘’Corona’’ kwa kuzingatia miongozo inayotolewa na wataalamu wa Afya.

Aidha Mhe. Rais alitumia fursa hiyo pia kuwahamasisha wafanya biashara kufuata Sheria na kanuni zote zilizowekwa na Halmashauri pia wananchi wote kuhakikisha wanashiriki katika suala la ulinzi na usalama kwa kufichua watu wenye nia ya kuvuruga amani.

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jobu Y. Ndugai (Mb) Jimbo la Kongwa, amemshukuru Mhe. Rais na serikali yake kwa kufanikisha upatikanaji wa fedha za kuendeshea miradi mbalimbali hususani ya Elimu, Afya, miundombinu na kadharika,katika jimbo la kongwa ikiwemo kata ya Kibaigwa.

Mheshimiwa Ndugai kupitia kwa Diwani wa kata ya Kibaigwa amewasilisha ombi la kuboreshewa huduma ya umeme kwani licha ya wakazi wengi kutounganishiwa umeme bado umeme uliopo hautoshelezi.  Ombi lingine ni la kupanuliwa kwa maegesho ya Magari katika mji huo wa Kibiashara ili kuwezesha wajasiliamali wengi kufanya biashara kwa ufanisi.

Akijibu changamoto hizo, Mhe. Rais ameahidi kuzishughulikia na ameahidi kuwa Serikali itaendelea kutoa fedha kwaajili ya miradi ya maendeleo. Na kuhusu kero ya maegesho ya magari ameeleza kuwa serikali kwa kushirikiana na sekta husika pamoja na Halmashauri ya Kongwa wanaendelea na jitihada za kutatua kero hiyo. Kwa upande wa tatizo la umeme Mhe. Rais ameahidi kuwa suala hilo pia lipo ndani ya uwezo wa serikali kwani waziri mwenye dhamana atashughulikia ndani ya kipindi kifupi.

Licha ya wananchi kutoizungumzia Migogoro ya Ardhi iliyopo katika kata ya Kibaigwa, Mheshimiwa Rais ametaja kuwepo kwa migogoro ya ardhi na hivyo ameahidi kuwa Waziri au Naibu wa Wizara husika atafika kushughulikia changamoto hiyo.

Mapokezi hayo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan yalihudhuriwa na umati wa wananchi na Viongozi mbalimbali waliokuwa wamejipanga kando ya barabara akiwemo, Mhe. Spika wa Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Katibu tawala wa wilaya ya Kongwa, Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kongwa, kamati ya ulinzi na usalama mkoa, kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Kongwa, viongozi wa Chama (CCM) mkoa na wilaya na wengineo.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.