• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Semina elekezi kwa waandishi wasaidizi na waendeshaji wa vifaa vya bayometriki katika zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura yaanza Kongwa

Imewekwa: September 22nd, 2024

Leo tarehe 22 Septemba semina maalumu kwa waandishi wasaidizi na waendeshaji wa vifaa vya bayometriki katika zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura imefunguliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kongwa Dkt Omary Nkullo katika ukumbi wa VETA na ukumbi wa shule ya Kongwa Sekondari.

Mamia ya waendeshaji vifaa vya bayometriki Pamoja na waandishi wasaidizi wamepata wasaa wa kupewa maarifa juu ya zoezi zima la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, pia wamekula kiapo kabla ya kutia Saini mikataba yao ya kazi husika, pamoja na kupatiwa elimu maalumu juu ya mambo mbalimbali yanayohusu zoezi husika.

Wataalamu mbalimbali kutoka tume huru ya uchaguzi wametoa somo la namna ya kutumia vifaa vya bayometriki Pamoja na afisa uhamiaji ambaye alitoa elimu ya uraia ili kuongeza uelewa kwa waandishi wasaidizi kumtambua raia anayestahili kushiriki zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura. 


Waandishi wasaidizi pamoja na waendeshaji wa vifaa vya bayometriki wakila kiapo kutunza siri katika zoezi la uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura.

Aidha akiongea na waandishi wasaidizi Pamoja na waendeshaji wa vifaa vya bayometriki, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt Omary Nkullo amesisitiza uadilifu kwa wahusika katika zoezi zima Pamoja na kuhakikisha wananchi wote watakaojitokeza katika zoezi hilo wanapatiwa ushirikiano ipasavyo ili zoezi hilo lifanikiwe kwa asilimia mia moja. Pia waendeshaji vifaa vya bayometriki wameaswa kuwa waangalifu na vifaa kuhakikisha wanavitunza katika siku zote za zoezi la uboreshaji daftari la wapiga kura kwani ni vifaa vya gharama kubwa na vinahitajika kuwa katika ubora huo huo waliovipokea kipindi watakapovirudisha zoezi litakapofikia tamati.


 

waendeshaji vifaa vya bayometriki wakipata mafunzo katika semina elekezi.

Semina hiyo elekezi kwa waandishi wasaidizi Pamoja na waendeshaji vifaa vya bayometriki itafanyika kwa siku mbili na zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura litaanza wilayani Kongwa siku ya tarehe 25 Septemba na kufanyika hadi ifikapo tarehe 1 Oktoba mwaka huu.


Imeandaliwa na 

Mbonea Masha

Afisa Habari Halmashauri ya wilaya ya Kongwa.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.