• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

SERIKALI INATAMBUA MCHANGO WA TAASISI ZA DINI - DAS KONGWA.

Imewekwa: November 19th, 2024

Katibu tawala wilaya ya Kongwa Bi Sozi Ngate amepongeza kanisa Katoliki la Mtakatifu Fransisco wa Asiz Kongwa kwa juhudi zake za kushirikiana na Serikali na kuongeza kuwa Serikali inatambua mchango wake katika kuleta maendeleo.

Bi Sozi ameyasema hayo  kwa niaba ya mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Mayeka Simon Mayeka katika uzinduzi wa albam yenye nyimbo Saba za Injili ya kwaya ya Mtakatifu Sesilia Kanisa Katoliki la Mtakatifu Fransisco wa Asiz Kongwa iliyoanzishwa mwaka 1973 ambapo ameipongeza kwaya hiyo kwa hatua waliyofikia ya kurekodi video kuwa ni uamuzi mzuri.

Aidha Bi Sozi amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wa Serikali wanasisitiza ushirikiano kati ya taasisi za dini na Serikali kwa ustawi wa Taifa kwani taasisi za dini licha ya  kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuchangia miradi ya maendeleo lakini pia zimekuwa zikisaidia kutatua changamoto mbalimbali katika jamii.

Vilevile Bi Sozi ameomba Viongozi wa Taasisi za dini kudumisha umoja na mshikamano na pia kumuombea Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kwa kazi kubwa anayozofanya lakini pia kuwaombea viongozi na Taifa kwa ujumla na Taifa kuwa na amani na utulivu wa kutosha.

Bi Sozi ameweka wazi kuwa jamii imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya mmomonyoko wa maadili na matukio mbalimbali lakini anawapongeza Viongozi wa dini Kwa mchango wao wa kukuza imani na kufundisha maadili kwa waumini wao na kusaidia kupunguza matukio hayo katika jamii.

Akijibu changamoto za kwaya ya Mtakatifu Sesilia Kongwa zilizosomwa katika risala maalum na Mwenyekiti msaidizi wa kwaya hiyo Bw John Charles, Bi Sozi ameeleza kuwa Ofisi ya mkuu wa wilaya ya Kongwa itachangia kulingana na itakavyobarikiwa hadi kumaliza changamoto hizo changamoto mojawapo  ikiwemo ni ukosefu wa kinanda.

Mbali na hayo katika hafla hiyo ya uzinduzi wa albam hiyo iliyohudhuriwa na viongozi na watu mbalimbali ndani na nje ya wilaya ya Kongwa bi Sozi ametumia fursa hiyo kuwasihi wananchi kutumia haki yao ya kikatiba kuhakikisha wanapiga kura siku ya tarehe 27 Novemba kuwachagua viongozi wao wa Mitaa.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAFUNZO KWA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI -JIMBO LA KONGWA. October 22, 2025
  • TANGAZO LA MAFUNZO KWA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA - JIMBO LA KONGWA. October 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGA KURA JIMBO LA KONGWA October 14, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini September 23, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • DC KONGWA AZINDUA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI NGAZI YA WILAYA

    October 24, 2025
  • KONGWA YATOA ZAIDI YA MILIONI 216 MIKOPO 10% AWAMU YA KWANZA 2025/2026

    October 23, 2025
  • DC KONGWA ASISITIZA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA

    October 14, 2025
  • DED KONGWA AZINDUA DARASA JANJA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KIBAIGWA

    October 09, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.