• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

SERIKALI WILAYANI KONGWA KUUNDA KAMATI MAALUMU YA KUSIMAMIA MIRADI

Imewekwa: August 12th, 2021

Na Stephen Jackson, Kongwa       

  Serikali wilayani Kongwa, imepanga kuunda kamati maalumu itakayohusika na usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa.

  Kauli ya kuundwa kwa kamati hiyo maalumu imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emmanuel, wakati akizungumza na wajumbe wa kamati kuu ya mbio maalumu za mwenge wa uhuru 2021 wilayani hapa, katika ukumbiwa Halmashauri ya wilaya ya Kongwa wakati wa kikao cha Tathmini ya shughuli za Mapokezi ya Mwenge kwa mwaka 2021.

  Kwa mujibu wa Mhe. Mwema, Kamati hiyo itakuwa ikifanya ufuatiliaji wa karibu kwa miradi yote inayotekelezwa wilayani hapa, ili kuwezesha upatikanaji wa taarifa sahihi zinazohusu Miradi yote inayoendelea.

  Kufuatia mpango huo, Mhe. Mwema amewaagiza wakuu wa Idara na vitengo ndani ya Halmashauri kuwa na ratiba ya kutembelea miradi yote ya maendeleo na kuitolea taarifa kila mwezi ikiwa ni pamoja na kuwajulisha wananchi. Katika taarifa zao, wakuu wa Idara, watapaswa kueleza changamoto walizozibaini kwa kila mradi na kupendekeza njia au mbinu bora za utatuzi.

  Kuhusu Miradi ya uwekezaji wa Madini mkuu wa Wilaya amewataka wawekezaji kushirikiana na viongozi wa serikali za vijiji wakati wa kufanya makubaliano ya tozo ili kuepuka tabia ya utoroshaji wa madini kwa kuwa kitendo hicho kinakwamisha maendeleo. Ameongeza kuwa wakati wa makubaliano baina ya viongozi wa vijiji na wawekezaji ni lazima Mwanasheria wa Halmashauri ashirikishwe kikamilifu.

 Ilikudhibiti tatizo la utoroshaji wa madini unaofanywa na baadhi ya watu wasio na uzalendo, Mhe. Mwema ameahidi kufanya kikao na wadau wa Madini wilayani Kongwa kwa lengo la kuwajengea uwezo  ili wilaya iweze kukusanya mapato kutokana na uwepo wa Madini wilayani Kongwa.

  Wakati huo huo Mhe. Mwema ametangaza kampeni ya kufyatua Matofali laki moja kwa kila kijiji ili kuwezesha ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo miradi ya elimu na Afya. Mhe. Mwema alitoa maelekezo hayo kwa wakuu wa shule za sekondari na walimu wakuu katika kikao kazi kilichofanyika ofisini kwake asubuhi ya trehe 11 Agosti 2021, na baadaaye kwa wajumbe wa kikao cha tahmini ya mapokezi ya Mwenge wa uhuru kwa mwaka 2021. 

  Wajumbe wa kamati mbalimbali za mapokezi ya mwenge wa uhuru walikutana tarehe 11 Agosti 2021 kutathmini shughuli mbalimbali zilizofanyika, ikiwemo uchambuzi wa taarifa za miradi, pamoja na mapato na matumizi.

Matangazo

  • TANGAZO LA MAFUNZO KWA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI -JIMBO LA KONGWA. October 22, 2025
  • TANGAZO LA MAFUNZO KWA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA - JIMBO LA KONGWA. October 22, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGA KURA JIMBO LA KONGWA October 14, 2025
  • Tangazo la kuitwa kazini September 23, 2025
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • DC KONGWA AZINDUA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI NGAZI YA WILAYA

    October 24, 2025
  • KONGWA YATOA ZAIDI YA MILIONI 216 MIKOPO 10% AWAMU YA KWANZA 2025/2026

    October 23, 2025
  • DC KONGWA ASISITIZA WANANCHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA

    October 14, 2025
  • DED KONGWA AZINDUA DARASA JANJA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KIBAIGWA

    October 09, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.