• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Serikali yashauriwa kubuni njia mbadala ya kuwasaidia Watu wenye ulemavu.

Imewekwa: May 4th, 2023

Na Stephen Jackson, KDC

Viongozi wa dini wameishauri serikali kutafuta njia mbadala ya kuwasaidia watu wenye ulemavu badala ya kuwakopesha fedha kwa kuwa wengi wao hawana elimu ujasiriamali.

Ushauri huo umetolewa Mei 4, 2023 na Mchungaji Kanoni Agripa Ndatila, Mkuu wa chuo cha Theolojia cha Mt. Philip kilichopo wilayani Kongwa Mkoani Dodoma, wakati wa mkutano wa kimataifa wa wakuu wa vyuo vya theolojia uliofanyika chuoni hapo ukihusisha mataifa matano.

Akifafanua hoja hiyo, Kanoni Ndatila alisema chuo hicho kinaendesha programu maalumu ya kutoa elimu juu ya namna ya kuwahudumia watu wenye ulemavu kwa miaka nane sasa, hivyo wamebaini kuwa njia bora ya kuwasaidia ni kuwafundisha ujuzi mbalimbali ili waweze kujitegemea.

Akizungumza muda mfupi baada ya kuhitimishwa kwa mkutano, Mchungaji Dkt. Daniel N.Karanja kutoka kanisa la Episcopal Marekani ameitaka jamii kubadili mtazamo kuhusu watu wenye ulemavu kwa kutambua umuhimu wao na kwamba jamii inahitaji mchango wao.

Kwa upande wake msemaji mkuu katika Mkutano huo Mchungaji Dkt. Emily Awino Onyango mkufunzi katika chuo kikuu cha Mt. Paul nchini Kenya aliwataka viongozi wa dini kutafsiri vizuri maandiko ili kuwezesha watu wenye ulemavu kupata ahueni ya Maisha. Katika wasilisho lake alisema endapo viongozi wa dini watatimiza wajibu huo, itasaidia kupunguza changamoto katika masuala mengine ya kijamii ikiwemo ukatili wa kijinsia. 

Akitoa maoni yake Kanoni Hilda Kabia Mkuu wa chuo cha Theolojia Msalato alisisitiza kuwepo na miundombinu wezeshi katika kila taasisi ili kupunguza adha kwa watu wenye ulemavu.

Naye Mratibu wa Mpango wa walemavu Mchungaji Naftaly Zabroni kutoka chuo cha Mt. Philip ameitaka jamii kuwajali walemavu ikiwa ni pamoja na kuwatembelea na kuwasaidia kwa hali na mali.

Kufuatia maudhui hayo, mchungaji Kanoni Edward Martin Komba Mkuu wa Chuo cha Mt.Marks kilichopo jijini Dar es Salaam akawashauri viongozi wa dini kufanya kazi kwa kushirikiana na viongozi wa serikali katika jitihada za kuboresha Maisha ya watu katika jamii. 

Awali Mkurugenzi wa programu ya walemavu nchini Bi. Wendy Broadbent raia wa Amerika alisema Tanzania inazo sera na sheria nzuri zinazolinda watu wenye ulemavu

Viongozi wengine wa mataifa ya Afrika walioshiriki kwenye mkutano huo ni pamoja na Mchungaji Kahwa Njonjo (DRC), Mchungaji Jesee Mutugi (Kenya) na Dkt. Pascal Bigirimana kutoka Burundi.

Mpango huo umefadhiliwa na Ofisi ya Global partnership ya nchini Malekani na unasimamiwa na wachungaji David Copley (USA) na Dkt. Daniel N. Karanja (Afrika)

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.