• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Spika aongoza mamia ya wakazi wa Kongwa na Viongozi mbalimbali Kuaga Mwili wa Mkurugenzi

Imewekwa: April 17th, 2018

Spika wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Kongwa Joab Ndugai April 16/2018 ameongoza mamia ya wakaziwa Kongwa na Viongozi mbalimbali Katika Ibada ya kuaga Mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhandisi Ngusa Izengo na kusafirishwa kuelekea kwao Chato Mkoani Mwanza

kwa Mazishi.

Akitoa Salamu za Rambirambi katika viwanja vya Halmashauri ya Kongwa Ndugai alisema,Hajawahi kufanya kazi na Mkurugenzi wa aina Ya Jinsi alivyokuwa Ngusa, kutokana na umahiri wake kwa kipindi alichokuwa katika Halmashauri hiyo,Kulikuwa na Utulivu katika vikao mbalimbali Tofauti na baadhi ya wakurugenzi waliwahi kufanya kazi katika halmashauri hiyo. "Hii ni kutokana na Hekima aliyokuwa nayo Ngusa." Alisisitiza.

Pia Ndugai alisema Eneo alilopatia ajali ni eneo ambalo linatakiwa kutizamwa kwa umakini kwani ni eneo hatarishi na limekuwa likisababisha ajali Mara kwa Mara. Aidha,Padri Alanus Ngonyani wa Parokia ya Kongwa akitoa mahubiri Katika ibada ya Kuaga mwili huo akitoa mahubiri Katika ibada ya Kuaga mwili huo aliwataka wanadamu kuhakikisha wanaishi na kutenda mema katika maisha ya Kila siku ili kujiandaa na Mauti kwani ni ahadi.

Katibu wa wabunge wa Dodoma Edwin Sanda ambaye ni mbunge wa Kondoa mjini akiwasilisha Salamu za Rambirambi kwa niaba ya wabunge Mkoa wa Dodoma alisema, Ngusa alikuwa mtu aliyependa ushirikiano na watendaji wenzake kwa ujumla Wamepoteza Mtu muhimu Katika Harakati za ujenzi wa Taifa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kongwa amemshukuru mkurugenzi wa Manispaa ya ubungo John Kayombo kwa namna alivyoguswa na Msiba huo na kutoa mchango wa Sanduku la Kwa ajili ya Kubebea mwili wa marehemu. "Hi inajidhihirisha ni Jinsi gani Ngusa aliishi kwa Kushirikiana na kugusa maisha ya watu" Ndejembi alieleza.

Dr.Abdulah Makame Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki akitoa salamu za Rambirambi amewapa pole wananchi wa Kongwa na kuwataka waendelee kumuombea Apumzike kwa Amani. 

Kadhalika Naibu Waziri Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa Mh.Josephat Kakunda Katika salamu hizo alisema, Ngusa alikuwa Mbunifu, mwadilifu,mchapakazi mzalendo na mwenye uaminifu mwadilifu,mchapakazi mzalendo na mwenye uaminifu Katika utendaji wake wa Kazi na kuwataka watendaji wengine kuiga mfano huo.

Ibada Hiyo ilihudhuriwa na Viongozi Mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahenge, Wafanyakazi wa Halmashauri hiyo, Wakurugenzi wa Wilaya za Jirani Gairo,mpwapwa Kondoa, na wakuu wa Wilaya hizo, Madiwani wa Halmashauri hiyo pamoja na Wananchi wa kutoka maeneo mbalimbali. 

Ngusa alizaliwa April 14/1972 na alifariki kwa ajali katika eneo la Makaravati mpakani kwa wilaya ya Kongwa na Chamwino usiku wa April 14/2018 kwa ajali ya Gari yake Kuangukiwa na Lori la Mafuta

"Bwana Ametoa na Bwana ametwaa na Jina la Bwana na lihimidiwe"

Amen.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.