• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

TAKUKURU WILAYA YA KONGWA YATOA ELIMU KWA JESHI LA POLISI.

Imewekwa: September 26th, 2024

Na Bernadetha Mwakilabi, Kongwa 

 

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Wilaya ya Kongwa imetoa elimu kwa Askari wa Jeshi la Polisi Wilayani Kongwa.

Semina hiyo imefanyika tarehe 25 Septemba katika ukumbi wa Polisi Jamii Kongwa ambapo Askari hao wameweza kujifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na utendaji wa kazi wa Taasisi hiyo pamoja na Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329 rejeo la mwaka 2022.

Akitoa elimu hiyo Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Kongwa Bwana Cosmas Shauri amesema kuwa majukumu ya Taasisi hiyo kwa ufupi ni Kuzuia na Kupambana na Rushwa, ambapo Taasisi hiyo inatekeleza jukumu la kuzuia Rushwa kwa kushirikisha Umma katika mapambano dhidi ya Rushwa hivyo jamii ikielewa vyema dhana ya mapambano dhidi ya rushwa basi kazi ya kuzuia rushwa itakuwa rahisi. Wananchi wakielewa vema wataweza kufuatilia miradi ya maendeleo katika maeneo yao na kutoa taarifa TAKUKURU mara wanapobaini uwepo wa vitendo vya rushwa, pia wananchi wakielewa ubaya wa rushwa itakuwa rahisi kukataa kujihusisha na vitendo hivyo.

Mkuu huyo wa TAKUKURU Wilaya ya Kongwa alieleza kuwa ofisi inazuia rushwa kwa kufanya tafiti na kupitia mifumo ya utendaji kazi ya Taasisi za Serikali, zisizo za kiserikali pamoja na mashirika ya umma ili kubaini mianya ya rushwa katika mifumo hiyo na kutoa mapendekezo kwa taasisi na mashirika husika jinsi ya kuziba mianya hiyo.

Akielezea kuhusiana na Kupambana na rushwa, Bw. Shauri alieleza kwamba baada ya kuwa vitendo vya rushwa vilishafanyika basi Taasisi hiyo inakuwa haina budi kupambana ambapo kunahusisha kufanya uchunguzi wa vitendo vya rushwa na kuwafikisha Mahakamani kwa kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka wale wote watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo.

Moja ya makosa yaliyofafanuliwa ni pamoja na kosa la kuomba na kupokea rushwa kinyume na sheria lililopo chini ya kifungu cha 15  cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na rushwa sura ya 329 rejeo la mwaka 2022, imeelezwa kwamba ni kosa kwa mtu yoyote mwenye mamlaka ya kutoa huduma fulani kuomba kitu chochote chenye thamani (fedha au mali) ili aweze kutoa huduma hiyo, au aache kutekeleza majukumu yake ya kikazi na kwamba kile kitu kinachotolewa kwa mtu huyo ili atimize au asitimize wajibu wake ndicho kinajulikana kuwa ni rushwa.

Aidha Bw Shauri alieleza kwamba kwa mujibu wa Kifungu cha 15 (b) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ni kosa kwa mtu yoyote kutoa rushwa kwa mtu yoyote mwenye mamlaka ya kutekeleza jukumu fulani ili atekekeze au asitekeleze jukumu hilo.

Kosa lingine ambalo alifafanua ni kosa linalotokana na kifungu cha 22 Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa sura ya 329 rejeo 2022 ambacho kinakataza matumizi ya nyaraka zenye maelezo ya uwongo kwa lengo la kumdanganya mwajiri, akifafanua kosa hili alitolea mfano wa mtumishi ambaye anatumwa kwenda safari ya kikazi na mwajiri wake ambapo anakuwa amepangiwa kwenda kufanya kazi hiyo kwa muda wa siku saba lakini kazi hiyo ikafanyika kwa siku tatu, na yeye akaendelea kuomba kiasi cha fedha ya siku saba nakuwasilisha maombi hayo kwa mwajiri wake, hiyo hati ya malipo aliyoomba malipo ya siku saba itakuwa ni nyaraka yenye maelezo ya uwongo kwa lengo la kumdanganya mwajiri wake.

Akifafanua kuhusiana na kifungu cha 29 cha sheria hiyo, Bw. Shauri anasema ni kosa kwa mtu yoyote kuchepusha mali za umma. ametolea mfano wa mfanyakazi kuhamisha mali ya ofisi na kwenda kuitumia kwa maslahi yake binafsi, mfano wa mali hiyo kuwa yaweza kuwa vifaa vya ofisi, magari, pikipiki na vaifaa vingine vinavyofanana na hivyo.

Kosa lingine linatoka kifungu (25) ambapo kifungu hiki kinahusiana na rushwa ya ngono kinachoeleza kuwa ni kosa kwa mtu yoyote mwenye mamlaka ya kufanya jambo fulani au kutekeleza wajibu fulani kushawishi au kuomba ngono ili aweze kutekeleza jambo hilo ambalo linahusiana na majukumu yake ya kila siku.

Vilevile Bw. Shauri amefafanua kuwa kifungu (27) cha Sheria hiyo kinahusu mtumishi wa Umma kuishi maisha ambayo hayalingani na kipato chake aidha kinahusu mtumishi wa umma kumiliki mali ambazo hazilingani na kipato chake.

Amefafanua kwamba iwapo uchunguzi wa awali utabainisha kwamba mtumishi fulani anamiliki mali zisizolingana na kipato chake, ofisi ya TAKUKURU itampatia mtumishi huyo Ilani ya kujieleza ambapo ataeleza mali alizonazo na jinsi alivyozipata na iwapo atashindwa kueleza kuwa ni jinsi gani amezipata mali hizo basi sheria itazitambua mali hizo kuwa zimepatikana kwa njia ya rushwa hivyo mtuhumiwa huyo akitiwa hatiani mahakamani mali hizo zitaweza kutaifishwa.  

Aidha akielezea umuhimu wa Jeshi la Polisi kupata elimu ya rushwa amesema elimu hii ni kwa ajili ya Askari wa Jeshi la Polisi kutojihususha na vitendo vya rushwa lakini pia ni kwa ajili ya wao kutoa ushirikiano wanapokutana na vitendo vya rushwa kwa kutoa taarifa katika ofisi ya TAKUKURU ili kufanyia kazi vitendo hivyo vya rushwa.


                                                                                                                       Ma-afisa wa jeshi la polisi wakisikiliza kwa makini mafunzo katika semina elekezi.

Nae Mkuu wa Dawati la Elimu kwa Umma ofisi ya TAKUKURU Wilaya ya Kongwa Bwana Severine Kisuda amesema kuwa asilimia kubwa ya maeneo yanayolalamikiwa ni wakati wa upelelezi wa makosa na makosa ya usalama barabarani ambapo amewasihi Jeshi la polisi kubadilika kwa kufanya kazi kwa weledi na uaminifu kuwasaidia raia kupata haki zao kwa wakati.

Kwa upande wake, Mkuu wa polisi Wilaya ya Kongwa Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Omary Mwanyika ameshukuru TAKUKURU kwa elimu ya Rushwa waliyoitoa na kuwataka Askari kufuata utaratibu wa kazi, aidha ameomba Takukuru kuendelea kushirikiana katika kutoa elimu kwa Askari ili wajue makosa ya rushwa na namna ya kuepukana nayo.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.