• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Wafanyabiashara wajengewa uwezo mabadiliko ya Sheria ya kodi

Imewekwa: September 6th, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Dodoma imewajengea uwezo wafanyabiashara wa Mamlaka ya mji mdogo wa Kibaigwa kuhusu mabadiliko ya Sheria za kodi Kwa lengo la kuondoa mkanganyiko wakati wa utekelezaji wa Sheria hizo.

Akitoa semina Kwa wafanyabiashara hao, Afisa Msimamizi kodi mwandamizi  ndugu Philipo Eliamini ametaja mabadiliko mbalimbali yaliyofanyika kwenye Sheria, na taratibu zinazotumika kufanya makadirio, na aina za kodi zinazopaswa kulipwa.

Aidha bwana Eliamini ametilia mkazo umuhimu wa utunzaji wa kumbukumbu za biashara ikiwemo matumizi "EFD".  Sanjali na hayo amewataka wafanyabiashara kusajili maghala na stoo wanazomiliki, na kuhakikisha wanadai risiti kila wanaponunua na kuuza  bidhaa.

Aidha Ndugu Eliamini ameongeza kuwa, endapo mfanyabiashara atanyimwa risiti Kwa bidhaa alizonunua atapaswa kutoa taarifa kwenye Ofisi za Mamlaka ya Mapato zilizo karibu naye ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa.

Kwa upande wake Afisa biashara wa Halmashauri ndugu Yonaza Mchome amewataka wafanya biashara kutoa taarifa Ofisi ya biashara pindi wanapofunga biashara zao badala ya ilivyozoeleka kwamba mfanyabiashara hutoa taarifa ya kusitisha biashara yake kwenye Ofisi za Mamlaka ya Mapato pekee.

"Ni vizuri unapofunga biashara, ni vizuri tukapata taarifa ofisi yetu ya biashara lakini pia ukatoa taarifa kwa wenzetu wa TRA". Alisema Ndugu Mchome.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Tech import & Export LTD. ya Kibaigwa inayojihusisha na usafirishaji wa nafaka Bi. Gath Marwa, amesema kwamba binafsi semina hiyo imemwezesha kujua aina za Kodi anazopaswa kulipa tofauti na alivyokuwa akijua awali na amewashauri wafanyabiashara kuacha kukwepa kodi, kwani kulipa kodi ni moja ya uzalendo.

Kwa mujibu wa miongozo ya TRA wafanyabiashara ambao mauzo yao ni chini ya milioni 14 kwa mwaka, ndio pekee wanaoruhusiwa kutumia vitabu  vya risiti vinavyoonesha Namba ya mlipa kodi (TIN) pamoja na taarifa zingine kuhusiana na biashara yake, na yeyote ambaye biashara yake  inazidi kiwango hicho anapaswa kutumia Mashine ya kielektroniki ya EFD.

Kwa upande wake Mkuu wa Kituo Cha Kodi Kibaigwa ndugu  Ezekiel Shekiyandumi amewakumbusha wafanyabiashara kujenga tabia ya kuandika barua za taarifa ya kusitisha biashara zao pindi wanaposhindwa kuendelea nazo ili kuruhusu  maafisa wa kodi kufanyia kazi taarifa hizo kwenye mfumo wa kodi.

Akifunga semina hiyo Diwani wa Kata ya Kibaigwa Mhe. Chande Mrisho amesema, karibu 30% ya Mapato ya Halmashauri hutoka kwenye Mamlaka ya mji mdogo wa Kibaigwa, hivyo amewahakikishia wawezeshaji wa semina hiyo kuwa yote waliyoelekeza watayafanyiwa kazi na kuitaka Mamlaka ya Mapato kuendelea kutumia busara ili kujenga mahusiano mema na wafanyabiashara.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.