• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

TUSIFUMBIE MACHO MATUKIO YA UKATILI.

Imewekwa: June 16th, 2025

Rai imetolewa kwa jamii kutofumbia macho matukio ya kikatili yanayotokea katika jamii ili kokomesha vitendo hivyo.

Rai hiyo imetolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Kongwa Bi. Sozi Ngate alipokuwa akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kongwa katika maadhimisho ya Siku ya ya familia Duniani yaliyofanyika katika Kata ya Makawa ambapo ameeleza kuwa katika kipindi cha Januari hadi Machi kumekuwa na matukio 6 ya ukatili ambapo kati yake kesi 3 zipo mahakamani na kesi 3 zinaendelea kufanyiwa uchunguzi na Jeshi la Polisi.

Aidha Bi Sozi Ngate amewasihi wazazi kuzidisha ulinzi na usalama kwa Watoto wenye umri wa kuanzia miaka 0-8, kuacha maneno ya maudhi, vipigo, pamoja na kuwapatia watoto elimu, huduma za Afya, lishe bora ili kuwaepusha watoto na changamoto mbalimbali.

Vilevile amefafanua kuwa baadhi ya sababu ikiwemo mafarakano na migogoro katika familia zimepelekea malezi duni kwa watoto pamoja na uangalizi hafifu hivyo kupelekea watoto kujilinda pamoja na kujitafutia mahitaji yao wenyewe, changamoto inayosababisha kuwa na kundi kubwa la watoto wa mitaani na kupelekea kundi hili kujiingiza katika vitendo visivyo na maadili katika maisha yao.

Naye Afisa maendeleo ya jamii Bi. Faraja Kasuwi ametaja kauli mbiu ya maadhimisho hayo 2025 kuwa ni "Mtoto ni malezi; msingi wa familia bora kwa Taifa imara" inayolenga kuwakumbusha wazazi na walezi jukumu lao la msingi kuwa ni malezi ya watoto ili kujenga msingi imara wa familia na hatimaye kuwa na Taifa imara la baadae.

Bi Kasuwi ameongeza kuwa wazazi Wana wajibu wa kuwalea watoto ili kujenga Taifa lenye watoto wanaojitambua, kujithamini na wenye maadili mema, na kuongeza kuwa wazazi wana wajibu wa kudumisha amani na upendo katika familia zao ili kuepusha migogogoro isiyo ya lazima inayoweza kusababisha watoto kukosa huduma muhimu za malezi na makuzi.

Akiongea kwa niaba ya wazazi Bi Herieth Mkopi wa kijiji cha Makawa amewasihi wazazi wengine kuzingatia suala la kuwapeleka watoto kliniki kupata chanjo, kupima uzito na Kujua kama wana maradhi yoyote yanayowasumbua ili wapatiwe huduma za kitabibu mapema.

Nae Yakobo Elias mwanafunzi wa shule ya Sekondari Makawa amezitaja haki za watoto kuwa ni pamoja na kuishi, kulindwa, kusomeshwa, kusikilizwa na kupatiwa mavazi, makazi na chakula.

Madhimisho hayo yalichagizwa na midahalo mbalimbali ikiwemo haki na usalama wa mtoto, malezi na makuzi, elimu ya kupinga ukatili, elimu ya lishe na uzazi salama, elimu ya Msaada wa kisheria na maelezo ya nishati Safi ya kupikia.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • TUSIFUMBIE MACHO MATUKIO YA UKATILI.

    June 16, 2025
  • DUWASA NA VEI WAKABIDHI MAHITAJI YA SHULE KWA WATOTO 105.

    June 13, 2025
  • DC. MAYEKA AFUNGA MAFUNZO YA UTHIBITI UBORA WA SHULE KATIKA WILAYA YA KONGWA

    June 02, 2025
  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.