• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 27 NOVEMBA 2024.

Imewekwa: November 27th, 2024

Tarehe 27 Novemba 2024 ni tarehe muhimu iliyosubiriwa kwa hamu kwani tukio muhimu la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa linafanyika. Wananchi wanapata fursa ya kuchagua viongozi wao watakaowahudumia kwa miaka mitano ijayo

Akizungumza na wananchi waliojitokeza kupiga kura Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka S. Mayeka ameeleza kuwa, "Wananchi ni wajibu wetu kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa Ili kuchagua viongozi watakaotuletea maendeleo." Mhe. Mayeka S. Mayeka ameyasema hayo katika kituo cha kupigia kura kilichopo Kongwa shule ya Msingi ambapo alipata wasaa wa kumchagua mwenyekiti wake wa Kitongoji.


Aidha msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Kongwa Dkt. Omary Nkullo baada ya kupiga kura, amewataka wananchi wajitokeze kwa wingi kwani zoezi ni la dakika chache na sababu siku husika ni siku ya mapumziko, basi wasikae nyumbani na kuacha kujitokeza kwa ajili ya kutimiza haki yao ya kikatiba. Akielezea namna zoezi linavyoendelea Dkt. Nkullo amesema, "Vituo vyote kwa kupigia kura viko wazi na Wananchi wanaendelea kujitokeza kushiriki zoezi la kupiga kura.

Kwa upande wake Katibu tawala wa Wilaya ya Kongwa Bi. Sozi Ngate ameeleza kufurahishwa na wepesi wa zoezi hilo na kuonyesha kupendezwa na wananchi kutoa kipaumbele kwa wazee na watu wenye ulemavu kuweza kupiga kura kwanza ili wasikae kwenye foleni ndefu. Akizungumza na wananchi Bi. Sozi alisema, "Nimeshiriki kiamilifu zoezi la kumchagua kiongozi atakayeniletea maendeleo, unasubiri nini?"

Mbunge wa Jimbo la Kongwa na spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai pia ameshiriki zoezi la kupiga kura na ameeleza umuhimu wa wananchi kutimiza haki yao ya kikatiba akitanabaisha kuwa maendeleo yanaanza na viongozi wa serikali za mitaa, ambao ndio wanaopeleka kero na hoja za wananchi Kwenda ngazi za juu za uongozi wa Serikali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. Mhe. White Zuberi baada ya kutimiza haki yake ya kikatiba ya kupiga kura alisema kuwa, "Mwenyekiti wa Kitongoji ni kiongozi wa karibu Sana na Wananchi ambaye ni rahisi kujua kero za wananchi na kuzipeleka mbele kwenye ngazi za juu za uongozi wa Serikali Ili kupatiwa utatuzi, hivyo ni muhimu Sana kushiriki uchaguzi Ili kuchagua kiongozi ambaye ataleta maendeleo."

Wananchi ambao wanaendelea kujitokeza katika vituo mbalimbali vya kupigia kura wanafurahishwa na muda mchache wanaotumia kupiga kura na kuondoka Kwenda majumbani kwao huku wengi wakifurahi kuchagua viongozi wanaowataka wawaongoze miaka mitano ijayo.

Mwananchi Shiriki zoezi la kupiga kura kuchagua kiongozi wa kukuletea maendeleo. Kura Yako ni muhimu.

Imeandaliwa na,

 Mbonea Masha

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini (W) Kongwa

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.