• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Utitiri wa vyombo vya watumia maji, Watajwa kuzorotesha jitihada za Serikali huduma bora za maji vijijini

Imewekwa: November 3rd, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emmanuel amesema ipo haja ya Serikali kupitia Taasisi ya RUWASA kuangalia upya namna ya kuwa na chombo kimoja cha Watumia Maji ili kuondokana na changamoto za usimamizi zinazoikabili sekta ya maji vijijini.

Aidha kupitia Hotuba yake alionya vikali matumizi ya fedha mbichi (zisizowekwa benki) jambo ambalo limekuwa likijitokeza kwenye baadhi ya vyombo vya watumia maji (CBWSO).

Mhe. Mwema alisema hayo wakati akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano mkuu wa wadau wa sekta ya maji wa nusu mwaka ulioratibiwa na Wakala wa maji na usafi wa Mazingira (RUWASA) Wilaya ya Kongwa Novemba 3, 2023 kuhusu hali ya upatikananji wa maji safi na salama Wilayani Kongwa na programu ya Lipa kwa Matokeo P4R.

Akiunga mkono Rai ya Mkuu wa Wilaya, Kaimu Meneja wa RUWASA Mkoa wa Dodoma Mhandisi Bazil Mwiserya alisema RUWASA inaendelea na jitihada za makusudi za kupunguza utitiri wa vyombo vya watumia maji ili kuboresha utoaji wa huduma bora za maji na kwamba ni Matamanio yake kuona Rai ya Mkuu wa Wilaya ya Kongwa inatekelezeka na hivyo kuifanya Kongwa iwe fursa ya wengine kujifunza.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri, Makamu Mwenyekiti Mhe. Richard Mwite na Diwani wa kata ya Mkoka alisema Licha ya changamoto ya Upungufu wa huduma ya maji katika baadhi ya maeneo, Halmashauri imekuwa ikipata ushirikiano wa kutosha kutoka RUWASA tangu Taasisi hiyo ilipojitegemea chini ya Wizara  maji na kwa kipindi chote wamekuwa wakiwasilisha taarifa kwenye vikao vya Baraza la Madiwani mara kadhaa kwa lengo la kupokea ushauri.

Akiwasilisha taarifa katika Mkutano huo wa wadau, Meneja Ruwasa Wilaya ya Kongwa Mhandisi Nyamwanja Bwire alibainisha changamoto mbalimbali zinazorudisha nyuma jitihada za Taasisi hiyo ikiwemo ukiukwaji wa makusudi wa miongozo na taratibu za uendeshaji wa huduma za maji vijijini, mwingiliano baina ya serikali za vijiji na vyombo vya watumia maji na uwepo wa maji chumvi chini ya ardhi hali inayoathiri upatikanaji wa maji ya kutosha.

Akitoa Mafunzo katika Mkutano huo Afisa Maendeleo ya Jamii RUWASA Mkoa wa Dodoma Bi. Prisilla Mkilanya alisema Kwa mujibu wa maelekezo ya Mkurugenzi mkuu wa RUWASA, kufikia Mwezi DIsemba, 2023 vyombo vya watumia maji mkoani Dodoma vinatakiwa kupunguzwa hadi kufikia walau 15 kwa kila Wilaya.

Kuhusu wazo la kuwa na chombo kimoja cha watumia maji, Bi. Mkilanya amesisitiza kuwa mchakato huo huenda ukachukua muda mrefu hivyo wakati ukiendelea  wa wadau watambue kuwa ni vema kuendelea kufanya kazi kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya maji na Usafi wa Mazingira namba 5 ya mwaka 2019, mada iliyofafanuliwa na Mwanasheria wa Halmashauri. Bwana Lenatus Pauline.

Akiwasisilisha mada katika Mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Kongwa Mkaguzi wa Ndani wa Halmashauri Bwana Jacob Lutana Mugusi alithibitisha kuwepo kwa changamoto ya matumizi ya fedha mbichi katika Kata za Mlali na Mtanana ambapo zaidi ya shilingi Mil. 22 hazikuwa na nyaraka halali za matumizi.

Kufuatia hoja ya Mkaguzi wa ndani, Ofisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Wilaya ya Kongwa ikiwakilishwa na Bwana Hamad Kibwana imetoa elimu ya Rushwa na athari zake kwa wadau wa maji, na kwamba Taasisi hiyo haipo tayari kufumbia macho vitendo vya Rushwa, ikiwa ni Pamoja na Matumizi ya Fedha mbichi.

Akiwakilisha chama cha Mapinduzi (CCM) Mwenyekiti wa chama Mwl. Abdi Mussa Matari alisema Ni vema Ruwasa kupitia vyombo vya watumia maji ikajitegemea kwa kukusanya mapato kikamilifu badala ya kuitegemea Serikali.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.