• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

Imewekwa: April 28th, 2025

Wananchi wa Wilaya ya Kongwa wameaswa kumshukuru kwa dhati rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kurejesha mikopo ya asilimia kumi ambayo ilisimama kutolewa kwa muda.

Hayo yameongewa na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Mayeka Simon Mayeka ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni mia mbili na sabini na saba kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Pia DC. Mayeka amewaeleza wanawake waliohudhuria katika hafla hiyo kuhusu bahati waliyonayo sababu anayeongoza nchi ni mwanamke kama wao na anafahamu changamoto zao kiundani bila hata kuambiwa, hivyo waitumie faida hiyo kuchangamkia fursa mbalimbali ambazo Mhe. Rais anawapatia ili kuunga mkono juhudi zake na kundi kubwa la wanawake kujikwamua kiuchumi.

DC. Mayeka ametengua uvumi ambao umekuwa ukisikika kuhusu fedha za mikopo ya asilimia kumi ambao baadhi ya wananchi wamekuwa wakisambaza kuwa fedha hizo hata vikundi visiporejesha havitadaiwa na katika mwaka wa uchaguzi hakuna kikundi kitakachodaiwa kwa kusema hu oni uongo na waelewe kuwa Uchaguzi ni jambo linguine na lenye umuhimu katika Taifa lakini mkopo ni swala linguine ambalo halihusiani na Uchaguzi hivyo wasidanganyane sababu marejesho ya fedha hizo yatapelekea na vikundi vingine kunufaika kwa wao pia kupata fedha hizo.

DC. Mayeka ameeleza kuwa ni nia njema ya Serikali kuona mikopo hiyo inatafsiriwa kwa mabadiliko ya maisha yanayoonekana waziwazi katika jamii. DC. Mayeka pia amepongeza baadhi ya vikundi ambavyo vilikopa na kurejesha kwa uaminifu na kuomba mikopo kwa awamu nyingine na kutoa rai kwa vikundi vingine kuiga mfano wa vikundi hivyo.

Akisoma taarifa fupi ya mikopo ya asilimia kumi ya Halmashauri, Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii ameeleza kuwa kama ilivyo ada Halmashauri ilichakata maombi ya vikundi yanayotumwa katika mfumo wa wezesha ambapo maombi 87 yenye thamani ya shilingi bilioni 2.6 yalitumwa kwenye mfumo na baada ya kamati kuchakata kwa kutumia kanuni za utoaji mikopo, kamati ilipendekeza na kuidhinisha mikopo kwa vikundi 21 ambapo fedha zimeshawekwa kwenye akaunti za vikundi husika.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi, Katibu Tawala wa Wilaya ya Kongwa Bi. Sozi Ngate ameeleza kuwa lengo la serikali ni kuwezesha na kusaidia wananchi kujikimu kimapato kwa kuwapatia mitaji inayopatikana katika mikopo hiyo. Na ameeleza kuwa kamati inahusisha vyombo mbalimbali ikiwemo vyombo vya usalama ili kuhakikisha haki inapatikana katika ugawaji mikopo pamoja na kusaidia katika urejeshwaji wa mikopo hiyo. Pia amewapongeza wanavikundi waliofanikiwa kupata mikopo na kuwakumbusha kufata kanuni na sheria pamoja na miongozo ambayo ipo katika mikataba yao waliotia Saini.

Akiongea kwa wakati wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa dkt. Omary Nkullo licha ya kuwapongeza wanavikundi waliopata mikopo hiyo isiyokuwa na riba, lakini pia amewakumbusha kuwa mikopo waliyopata sio zawadi bali ni mikopo inayotolewa kutokana na agizo la Serikali kuwa fedha zinazotokana na kodi za wananchi asilimia kumi itolewe ili kukopesha makundi maalum ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu na inatakiwa irejeshwe ili na vikundi vingine vinufaike na mikopo hiyo ili kusudi mikopo hiyo iwafikie watu wengi zaidi.

Akizungumza baada ya kupokea mkopo, Bi. Debora Boma ambaye ni mwanakikundi wa kikundi cha Nyemo Group kinachojishughulisha na ufugaji wa Samaki kinachopatikana Kata ya Kibaigwa, ameeleza furaha ya kikundi kupata mkopo na kutoa shukrani zake za dhati kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kurejesha mikopo hiyo na kuahidi kuwa mkopo huo utafanya kazi iliyokusudiwa na fedha walizokopa zitarejeshwa kwa wakati kama jinsi ambavyo mkataba wa mkopo unavyoelekeza.

Naye Mohamed Said, Mwenyekiti wa kikundi cha Mshikamano Mtanana Group kinachojishughulisha na kilimo cha umwagiliaji ametoa shukrani zake za dhati kwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na uongozi wa Halmashari ya Wilaya ya Kongwa kwa mchakato mzima uliojikita katika haki ambao umepelekea vikundi vyenye sifa kupata mikopo hiyo, Bw. Said ameeleza kuwa ni dhima ya kikundi kubadili taswira ya kuwa kilimo ni cha wazee na watu wanaostaafu kwa kufanikiwa katika sekta hiyo kama vijana ili kuwa mfano kwa vijana wengine kujikita katika shughuli hiyo na kuacha kulalamika kuwa hakuna ajira.

Hii ni awamu ya pili ya utoaji wa mikopo ya asilimia kumi ambayo kwa awamu ya kwanza vikundi hamsini na nne vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vilikabidhiwa shilingi milioni mia tano sitini na tano ambapo katika awamu ya pili, vikundi ishirini na moja vimekabidhiwa shilingi milioni mia mbili sabini na saba laki tatu tisini nan ne n amia nne themanini nan ne kama inavyoelekezwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuwa Halmashauri zitoe asilimia kumi ya mapato yake ili kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa dhumuni la kuinua maisha ya wananchi na kuwaongezea kipato.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.