• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

VIKUNDI KONGWA KUPEWA SHILINGI MILIONI MIA TANO NA SITINI NA TANO

Imewekwa: November 17th, 2024

Vikundi Wilayani Kongwa vimekabidhiwa hundi ya shilingi milioni mia tano na sitini na tano katika awamu ya kwanza ya ugawaji mikopo. Mikopo hiyo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu Inaelekezwa na chama cha Mapinduzi kupitia ilani yake kuhakikisha Maisha ya wananchi yanainuliwa kupitia kupelekwa kwa mikopo ya asilimia kumi kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Vikundi Hamsini na nne vimepatiwa mkopo kwa awamu ya kwanza ambapo uteuzi umefanyika vizuri hadi kupelekea vikundi hivyo kuchaguliwa ili kunufaika na mikopo hiyo.

Mgeni rasmi pamoja na viongozi wengine wa Serikali wakikabidhi hundi yenye thamani ya mikopo iliyokabidhiwa wa vikundi.

Akiongea wakati wa kukabidhi mikopo hiyo, mgeni rasmi mhe. Mayeka S. Mayeka, Mkuu wa Wilaya ya Kongwa ameeleza kuwa nia ya mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuinua hali ya kiuchumi ya wananchi ni njema kwani milioni mia tano ingeweza kujenga vituo vya afya, madarasa, na miundombinu mingine lakini imeenda kutolewa kwenye vikundi ili wananchi wainuliwe hali yao ya kiuchumi.

Mgeni rasmi Mhe. Mayeka S. Mayeka akihotubia wanavikundi wakati wakisubiria kupatiwa mikopo.

Mhe. Mayeka amewasifu wenye vikundi vinavyofanya vizuri katika kurudisha mikopo na kutolea mfano vikundi ambavyo vilishakopa na kurudisha mikopo kwa uaminifu hivyo kupelekea kupata mkopo kwa awamu nyingine mwaka huu.

Moja ya vikundi hivyo ni kikundi cha bodaboda ambacho DC. Mayeka ameeleza kuwa kimefanya vizuri huko nyuma katika marejesho hivyo kufanya kupata mkopo kwa awamu nyingine na ameonyesha matamanio yake kuona kikundi hicho kikifikiria mbali zaidi ya bodaboda na kuendelea zaidi kwenye sekta hiyo ya usafirishaji.

Aidha Mhe. Mayeka ametoa rai kwa wanavikundi kuhusu marejesho ya mikopo ambayo bado baadhi ya vikundi havijarudisha na amewaasa kuondoa mtazamo uliokuwa mwanzoni kuwa fedha ya serikali ni ya kutumia pasi kurudisha. Pia Mkuu wa Wilaya ameelezea tatizo la migogoro kwa vikundi pale ambapo wanapata pesa hizi za mikopo na kueleza kuwa mafanikio hayawezionekana kwa njia hiyo ya migogoro mara pale ambapo vikundi vinawekewa pesa hizo kwani hii hupelekea vikundi kuvunjika na kuingia katika madeni.

DC. Mayeka amemaliza kwa kushauri wanavinkundi wafanye vizuri katika miradi yao kwa kutumia vizuri pesa walizopewa ili waweze kurejesha mikopo hiyo na kufanya Wilaya ya Kongwa kuwa Wilaya ya mfano katika ufanisi wa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, pia amewaasa vijana wenye fani wakimbilie fursa hizi za mikopo na wasiendelee kulalamika kuwa hakuna ajira na hakuna mitaji kwani serikali inatoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya mikopo ili kuwezesha wananchi wake wajikwamue kiuchumi.

Kwa upande wake Mbunge na spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiongea na wanavikundi amerejelea msemo wa, “Kama umezaliwa maskini, huna wa kumlaumu, ila ukifa maskini wakulaumiwa ni wewe mwenyewe.” Wakati akisisitiza kuwa mikopo hii ni fursa mahsusi kwa wananchi kujikwamua kutoka kwenye janga la umaskini na kuinua Maisha yao kiuchumi. Pia ameongeza kuwa matajiri wengi wametumia mikopo kuongeza utajiri wao hivyo hata wanavikundi wakitumia mikopo hii kwa uaminifu kutekeleza mipango waliojiwekea basi ni dhahiri kuwa watanufaika nayo.

Dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu lilifunguliwa rasmi tarehe 1 Oktoba mwaka huu kwa ajili ya vikundi kuomba fursa ya mikopo hiyo.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.