• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

Imewekwa: May 5th, 2025

Timu ya wataalam kutoka Idara ya maendeleo ya jamii imefanya ziara ya ufuatiliaji na tathmini kwa vikundi 47 vya Kata 16 vilivyonufaika na mkopo awamu ya kwanza Wilayani Kongwa kwa lengo la kuhakiki Miradi ya vikundi hivyo ili kujionea mwenendo wa miradi hiyo, changamoto na mafanikio ili kuwashauri waweze kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Bwana Alphonce Mkwizu Afisa Maendeleo ya Jamii ameeleza kuwa tathmini na ufuatiliaji wa fedha hizo za 10% ya Halmashauri kwa wanawake vijana na watu wenye ulemavu imeonesha kuwa kuna changamoto nyingi katika shughuli mbalimbali za kiuchumi zinazofanywa na vikundi zikiwemo shughuli za Kilimo cha umwagiliaji wa mazao ya biashara, maduka ya Dawa, maduka ya nguo, viwanda vidogo vidogo, maduka ya chakula, ufugaji, usafirishaji nk.

Aidha Ndg Mkwizu amesema kuwa changamoto zilizobainika ni pamoja na vikundi kubadili matumizi ya fedha ya mkopo bila kutoa taarifa kwa mtendaji na menejimenti akitolea mfano baadhi ya vikundi vilivyoomba fedha kwaajili ya kununua pikipiki lakini vikaenda kufanya biashara ya kununua na kuuza mazao.

Aidha Ndg Mkwizu ameongeza kuwa changamoto nyingine ni vikundi kushindwa kuweka akiba, kuwepo kwa migogogoro baina ya wanavikundi na kufanya kazi kwa mazoea bila kushirikisha wataalam kama vile maafisa ugani,maafisa biashara na viongozi wao wa Vijiji ili kuwasaidia kutatua changamoto wanazokutana nazo na kuwasaidia kupata matokeo bora zaidi ya kuwawezesha kupata marejesho.

Ndg. Joseph Mshana Afisa maendeleo ya jamii katika kutatua changamoto hizo amesisitiza wanavikundi kujisimamia katika kuweka akiba kwa kutekeleza agizo la kimwongozo ili kujiandaa na kujenga msingi mzuri wa marejesho unaotarajia kuanza Mei 8 na kuwakumbusha wafanye kazi kama walivyopanga katika katiba zao za vikundi na watumie fursa hiyo inayotolewa na Serikali kuhakikisha wanajikwamua na hali za maisha walizonazo.

Pia Ndg Mshana amewataka wanavikundi kushirikisha viongozi kwa kila hatua ya utekelezaji wa shughuli zao, kuweka kumbukumbu ya risiti ya kila kifaa wanachonunua ili kujenga uaminifu na kusisitiza kutumia vizuri fursa hiyo ya fedha za mkopo walizopata kwani watu wengi wanatamani kupata fursa ambazo wamezipata.

Mkuu wa Divisheni ya maendeleo ya jamii Wilaya ya Kongwa Bi. Paskalina Duwe ameagiza maafisa maendeleo ya jamii Kata kufuatilia vikundi kuhakikisha vinatekeleza maagizo yote yanayotolewa katika vikao pamoja na kutatua changamoto zinazokabili vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika kurejesha mikopo.

Kwa upande wao baadhi ya wanavikundi wametaja changamoto wanazokutana nazo kuwa ni mifugo kuugua hadi kufa, pamoja na mabadiliko ya bei ya kununulia mifugo hali inayopelekea kuwa na idadi ndogo ya mifugo au kununua mifugo ambayo haina ubora.

Bi Elizabeth Chidabile kutoka kikundi cha Mtazamo Chanya kilichopo kijiji cha Makawa kinachojishughulisha na Kilimo cha umwagiliaji mbogamboga na matunda kilichopatiwa mkopo wa shilingi milioni 21.4 anasema kuwa awali walilima kienyeji hawakupata mazao bora lakini baada ya Afisa ugani kuwapa elimu wameanza kulima kitaalam zaidi na mazao yameongezeka.

Pamoja na hayo wanavikundi hao wameishukuru Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia mikopo hiyo ambayo imesaidia kuwa na mitaji ya kufanya biashara na kujikwamua kiuchumi kwa kujiajiri, kuwa na makazi bora, kusomesha watoto, kukidhi mahitaji mengine ya familia na kutoa ajira kwa wanajamii.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.