• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Viongozi wa Kata na vijiji watakiwa kuitisha mikutano ya Kisheria

Imewekwa: May 15th, 2024

Na Stephen Jackson, Kongwa DC

Katibu Tawala Wilaya ya Kongwa Bi. Sozi Ngate amewataka viongozi wa Serikali za Kata na vijiji kuitisha mikutano ya kisheria ili kuwapa taarifa mbalimbali wanananchi, ikiwemo mapato na matumizi.

Bi. Ngate amesema hayo wakati akihutubia Wananchi wa Kata ya Chitego akiwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Familia duniani yaliyofanyika Kijiji cha Chitego kwa ngazi ya Wilaya Mei 15, 2024.

Wa pili kushoto ni Katibu Tawala (W) Bi. Sozi Ngate akishiriki Maadhimisho kama mgeni rasmi.

Akijibu miongoni  mwa kero za Wananchi kuhusu migogoro ya ardhi, Bi. Ngate alisema ni lazima uchunguzi ufanyike kuhusu tuhuma za kukodishwa shamba la kijiji na fedha kutumiwa nje ya taratibu, huku akiwataka Wananchi kuwa mstari wa mbele kushiriki mikutano na vikao vinavyoitishwa na viongozi wa vijiji na Kata " Suala la shamba la Kijiji tutaleta mkaguzi wa ndani ajiridhishe: Na kama kuna ubadhirifu tutachukua hatua, hakuna aliye juu ya Sheria". Alisema Ngate.

Sanjari na hayo amewataka Wananchi kuzingatia malezi bora kwa watoto wao, ikiwa ni pamoja na kuchangia chakula ili watoto wao waweze kusoma kwa furaha, huku akikemea Suala la utoro shuleni.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Makundi Maalumu Bi. Paskalina Duwe alisema kupitia picha kutoka kwa watoto, hali ya malezi kwa watoto kwa Sasa ni changamoto, hivyo ni lazima tofauti kati ya wazazi ziwekwe pembeni ili kuepuka kuathiri maendeleo ya watoto kwa kudumisha amani na upendo wa familia.

Bi. Paskalina Duwe Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii Kongwa

Naye Diwani wa Kata ya Chitego Mhe. Peter Y. Kalunju alitoa pongezi kwa Serikali kwa kutekeleza miradi mbalimbali katika Kata hiyo ikiwemo mradi wa maji wenye thamani ya shilingi milioni 147 uliopo kitongoji cha Mgoroka, Kijiji cha Ngutoto ingawa ameiomba Serikali kutatua changamoto ya barabara inayounganisha Kijiji cha Leganga na Chitego kwani kwa Sasa Wananchi wanatumia gharama kubwa kuzungukia Kata ya Zoissa wakati ipo barabara hiyo ya mkato.

Diwani wa Kata ya Chitego Mhe. Peter Kalunju akiwasilisha kero ya Barabara mbele ya meza kuu na Wananchi.

Akizungumzia mikakati ya mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia, Afisa wa polisi anayeshughulikia dawati la Jinsia, D/SGT Zaibabu Zuberi Halfan alisema lazima familia ziache malumbano ili kujenga familia bora.

D/SGT Zainabu Zuberi Halfan - Mkuu wa Dawati la Jinsia Polisi Kongwa akizungumza na Wananchi.

 Akizungumza na Wananchi Afisa Tarafa wa Tarafa ya Zoissa Bwana Denis Mbawi Semindu aliwataka Wananchi wa Kata hiyo kutoa ushirikiano wa Kutosha kwenye Zoezi la Mafunzo ya Jeshi la Akiba yanayotarajia kufanyika katika Kata hiyo.

Katika Maadhimisho hayo, Wananchi wamewasilisha kero mbalimbali ambazo viongozi wameahidi kuzishughulikia kikamilifu.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.