• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

WACHIMBAJI MADINI TAMBUENI NAFASI YA MWEKEZAJI.

Imewekwa: July 4th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mheshimiwa Mayeka Simon Mayeka ametatua mgogoro baina ya mwekezaji na wachimbaji wa madini katika mgodi uliopo katika Kijiji cha Iduo.

Akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama Mhe. Mayeka amekutana na makundi ya wachimbaji pamoja na uongozi wa Kata ya Iduo ambapo amesisitiza upelelezi ufanyike kubaini ukweli juu ya chanzo cha mgogoro uliotokea baada ya kijana ambaye alipigwa na mlinzi wa mgodi huo akishutumiwa kutorosha madini hali iliyopelekea vurugu mgodini hapo.

Aidha DC Mayeka amekemea vikali kitendo cha wachimbaji madini kujichukulia sheria mkononi akigusia tukio la wachimbaji kumnyang'anya silaha mlinzi wa mgodi huo na kwenda kuvamia nyumba ya mwekezaji na kufanya uharibifu wa mali na kueleza kuwa kitendo hicho ni uvunjaji wa sheria na hakikubaliki.

Mheshimiwa Mayeka pia amekemea suala la utoroshaji wa madini kuwa lilaweza kupelekea kufungwa kwa leseni ya mwekezaji na kusababisha upotevu wa mapato na kuwataka wachimbaji na mwekezaji kila mmoja kwa nafasi yake kutambua mipaka yake katika kazi ili kudumisha amani.

Pamoja na hayo mhe. Mayeka amemuagiza mwekezaji kujenga choo, afisa madini kusimamia usalama wa machimbo hayo na Afisa mazingira Wilaya ya Kongwa kuhakikisha uwepo wa vyoo bora kabla ya kufungua machimbo hayo ya madini ambayo yalifungwa baada ya kutokea kwa vurugu hizo.

Nae Diwani wa kata ya Iduo Mhe. Valentino Seng'unda amewataka wachimbaji wa madini wanaotoka kijiji cha Chamkoroma kutambua na kuheshimu uongozi wa Serikali ya Kijiji na kuwataka waache uchochezi na wafanye kazi kwa utaratibu na kupata riziki ya halali.

Akizungumza baada ya kikao, Afisa mazingira Wilaya ya Kongwa Bw. Godfrey Mujairi amesema Wilaya ya Kongwa ina maeneo makubwa ya kuchimba madini lakini mapato yake yapo chini kutokana na utoroshaji wa madini hayo, hivyo amewaomba wachimbaji na wawekezaji kutii sheria na taratibu za uchimbaji madini.

Akielezea mazingira ya vurugu hizo mwekezaji wa mgodi huo wa madini Bwana Hussein Mohamed amesema mlinzi alimkamata mchimbaji mdogo (ndugu Given Samson mkazi wa Chamkoroma ) akitorosha madini usiku mnamo saa 9 usiku na kuamua kumuadhibu kwa kumpiga na kumsababishia majeraha hivyo baada ya tukio hilo wachimbaji wengine waliamua kumpora mlinzi silaha ambayo aliifatilia na kuikabidhi katika kituo cha Polisi mlali lakini baada ya hapo wachimbaji hao walivamia nyumbani kwake na kufanya uharibifu.

Mpaka kufikia mwisho wa kikao hicho wachimbaji wawili wakazi wa Chamkoroma ndugu Perezi Maduwilu na Juma Mpemba wanashikiliwa na jeshi la Polisi kwa upelelezi zaidi kwa kusababisha uvunjifu wa amani na utoroshaji wa madini mgodini hapo.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • ECOKAZI WATOA MAFUNZO KUHUSU BIASHARA YA KABONI

    July 24, 2025
  • WASIMAMIZI WA AFYA WANOLEWA UDHIBITI NA UTENGANISHAJI TAZIHA.

    July 23, 2025
  • MWENYEKITI KIJIJI CHA MLANJE ARUDISHWA MADARAKANI.

    July 21, 2025
  • DED KONGWA APONGWEZWA UTOAJI MIKOPO 10%.

    July 18, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.