Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Wadaiwa fedha za mikopo ya 10% watakiwa kurejesha

Imewekwa: October 21st, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Kamati ya Fedha uongozi na Mipango Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma Imewataka viongozi wa vijiji na Kata kusimamia kikamilifu urejeshwaji wa fedha za serikali zilizotolewa kwa wajasiriamali kupitia mikopo itokanayo na asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe . White Zuberi Mwanzalila, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhe. Richard Mwite ambaye ni Diwani wa Kata ya Mkoka, ameviagiza vikundi vyote ambavyo havijarejesha fedha kufanya hivyo kabla ya Tarehe 31 Oktoba, 2022.

Kamati hiyo chini ya Mhe. Mwite ilitoa agizo hilo wakati wa ziara ya siku mbili ya ukaguzi wa miradi inayotekelezwa Wilayani Kongwa katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023.

Maamuzi hayo yanafuatia baada ya vikundi hivyo kushindwa kufanya marejesho ndani ya muda wa mkataba, ambapo kwa mujibu wa kanuni, vikundi hutakiwa kurejesha fedha katika kipindi cha miezi kumi na mbili.

Aidha kamati ilisikitishwa na taarifa kutoka taarifa ya Afisa Mtendaji Kata ya Sagara Bwana Abdunasil Mboya kudai kuwa baadhi ya wanakikundi wa kikundi cha Furaha kilichopo Kata ya Sagara, wametoroka na fedha za kikundi, hivyo kamati imemtaka Afisa huyo kuhakikisha wanakikundi hao wanapatikana na kurejesha fedha.

Katika ziara hiyo Vikundi mbalimbali vilitembelewa  Ikiwa ni pamoja na Furaha kutoka Kata ya Sagara na Upendo kutoka Kata ya Chiwe ambavyo Kila kimoja kilikopeshwa shilingi 4,000,000.00 ambapo kikundi cha Furaha kilikuwa kikidaiwa1,935,000.00 wakati kikundi cha Upendo kikidaiwa shilingi 2,890,000.00 hadi siku ya ukaguzi.

Wakati huo huo Kamati ilipongeza jitihada za kikundi cha Omega Cha Vijana wa boda boda  Kata ya Sagara na kikundi cha Nguvu kazi - Vijana kilichopo Kata ya Chiwe kinachoendesha kilimo cha umwagiliaji kwa mkopo wa shilingi milioni tano, ambapo kwa mujibu wa uongozi wa kikundi hicho, vijana hao huzalisha mboga mboga  serikali na kusambaza katika masoko ya ndani na nje ya Mkoa wa Dodoma.

Bibi Doricus Ndugai Mwenyekiti wa kikundi cha Upendo alidai kuwa, kutokana na hali mbaya ya hewa kikundi kilipata hasara baada ya kushindwa kuendesha shughuli zake, hivyo Ili kutekeleza agizo la kamati wanakikundi wanalazimika kugawana deni hilo na kuhakikisha wanarejesha fedha kabla au  ifikapo Tarehe 31 Oktoba, 2022.

Katika hatua nyingine Kamati ilifanya ukaguzi wa jengo la zahanati ya Kijiji cha Majawanga ambapo linalojengwa kwa nguvu za wananchi linalokadiriwa kuwa na thamani ya Shilingi 60,000,000.00 pindi litakapokamilika.

Katika ukaguzi huo Kamati ilipongeza wananchi na viongozi hao kwa ushirikiano wa dhati wa kuchanga fedha na kuanzisha ujenzi.

Katika taarifa yao wananchi hao walivainisha sababu zilizowasukuma kulingana na kuanzisha ujenzi huo kuwa ni kutokuwepo huduma za Afya katika maeneo ya karibu, hali inayowalazimu kufuata huduma hizo maeneo ya mbali.

Kwa kauli Moja kamati iliunga mkono jitihada hizo na kuahidi kushirikiana na wananchi wa Majawanga kukamilisha ujenzi wa Zahanati hiyo.

Kwa mujibu wa Afisa Mtendaji wa Kata ya Sagara, kikundi cha Furaha tayari kimeanza kurejesha fedha wanazodaiwa ingawa baadhi ya wanakikundi bado hawajapatikana.


Matangazo

  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.