• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

WAFUGAJI WALIA WIZI WA MIFUGO KONGWA.

Imewekwa: January 3rd, 2025

Wafugaji katika Kata ya Sejeli wilayani Kongwa wameiomba Serikali kuingilia kati suala la wizi wa mifugo unaoendelea katika Kata hiyo hali inayowapa hofu na kukatisha tamaa katika shughuli hiyo.

Wakiongea mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mheshimiwa Mayeka Simon Mayeka ambaye pia ni Mwenyekiti wa ulinzi na usalama wilaya wamesema kuwa pamoja na changamoto za malisho, maji, majosho, wataalam na masoko lakini kumekuwa na changamoto kubwa ya wizi wa mifugo kama Ng'ombe na Mbuzi ambapo mfugaji mmoja anaweza kuibiwa hadi mara tatu mfululizo hivyo wanaomba nguvu ya ulinzi na upelelezi, ili kuwabaini wezi wa mifugo hiyo ili waweze kufanya shughuli zao za ufugaji kwa amani na uhuru.

Aidha, wakitoa kero zao, wafugaji hao wameeleza kuwa wizi wa mifugo ni changamoto kubwa inayowakabili wafugaji na inapelekea kwa wingi wao kuogopa kufuga sababu hata ulinzi wa sungusungu wanaowatumia hausaidii kwani inasadikika kuwa sungusungu hao wamekuwa wakitoa siri za wafugaji na kupanga mipango ya wizi.

Sambamba na hayo wafugaji hao wameweka wazi kuwa wanaomba utaratibu wa utoaji vibali urejee ule wa awali yaani kibali kitoke Kijiji ambacho mfugo unatoka kwenda mnadani na kutoka mnadani kwenda kijiji ambacho mfugo unaenda ili kuendelea kuwabana wezi wa mifugo kwani vibali kwa Sasa vinatolewa mnadani tu.

Awali ya yote kabla ya kutoa majibu juu ya malalamiko hayo Mhe. Mayeka alitumia wasaa huo kuendesha kura ya siri kwa wafugaji kupiga kura kuwabaini wezi wa mifugo kwa majina na nafasi zao ili kuwachunguza na kuwachukulia hatua zaidi pindi watakapopatikana na hatia ya makosa ya wizi wa mifugo.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa mhe. Mayeka S. Mayeka akitolea ufafanuzi hoja zilizoibuliwa kwenye kikao.

Vilevile Mhe. Mayeka ametoa mikakati ili kudhibiti wizi huo ikiwemo kuweka kizuizi (Barrier) kwaajili ya kukagua magari yanayotoka wilaya ya Kongwa kwenda wilaya za jirani, na kuwataka wananchi kwa kushirikiana na viongozi wa vijiji husika kuweka doria ya sungusungu kwa kuwatumia Askari wa Jeshi la Akiba ambao ni waaadilifu ili kulinda maeneo yao.

Diwani wa Kata ya Sejeli Mhe. Chilingo Ng’hambi Chimeledya akiongea na wananchi wa Kata ya Sejeli katika kikao

Licha ya kuwataka wananchi kutokujichukulia sheria mkononi pindi watakapowabaini wezi hao lakini amewataka wafugaji na wananchi kushirikiana kwa pamoja kutokomeza wizi wa aina yoyote na wizi wa mifugo kwani wezi wakitawala ufugaji utakuwa mgumu na ametoa rai kwa wananchi kutoka kila Kijiji ndani ya Kata wanapofanya vikao, ajenda kubwa iwe ya usalama.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.