• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

WAHANDISI WASIO NA MIPAKA KUFADHILI BAISKELI WANAFUNZI WANAOTEMBEA UMBALI MREFU.

Imewekwa: December 20th, 2024

Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Kongwa Bi Magreth Temu amekabidhi baiskeli 35 kwa wanafunzi wa shule ya Sekondari Banyibanyi wanaotembea umbali mrefu kwenda shule kutokea Kijiji cha Mkutani takribani kilomita Saba.

Baiskeli hizo zilizokabidhiwa ni sehemu ya ufadhili kutoka kwa Wahandisi wasio na Mipaka kutoka Marekani (USA Engineers without borders) zikiwa na lengo la kuondoa vikwazo na changamoto za elimu zikiwemo utoro unaotokana na kutembea umbali mrefu kwa wanafunzi wa shule za Sekondari.



Akiongea wakati wa kukabidhi Baiskeli hizo Bi Temu ametoa shukrani kwa Wahandisi wasio na Mipaka kwa kusukuma gurudumu la elimu katika Wilaya ya Kongwa kwani licha ya baskeli hizo wameweza kujenga nyumba ya mwalimu, matundu ya vyoo 12, miundombinu ya kuvunia maji na chumba cha kompyuta kwaajili ya kusaidia wanafunzi kusoma masomo ya Tehama katika shule ya msingi Mkutani ambapo ameongeza kwa kuwa baiskeli hizo ziwe chachu ya kuongeza bidii ya masomo kwa wanafunzi.

Aidha Mwl. Magreth Temu ameshukuru viongozi wa wilaya ya Kongwa hususani Mbunge wa Jimbo la Kongwa Mhe. Job Ndugai kwa kutoa kipaumbele kwa wanafunzi wanaotoka Kijiji cha Mkutani kupata baskeli hizo kwani ni wanafunzi wa maeneo mengi wanahitaji msaada huo na kuwataka wazazi kuhakikisha wanazitunza baiskeli hizo ili ziwe na faida iliyokusudiwa.


Pamoja na kuhimiza uchangiaji wa Lishe mashuleni pia Mwl. Temu amewataka wanafunzi wote waliofeli mtihani wa darasa la saba mwaka 2024 kurudia darasa la saba mwaka 2025 ili kuendelea na masomo, na kuwasihi wazazi kujitokeza kuwaandikisha shule wanafunzi wenye ulemavu ili nao wapate elimu.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Hogoro Mheshimiwa Mtwanga Sadala amewataka wenyeviti wa vitongoji kushirikiana na wazazi kushughulikia utoro wa wanafunzi mashuleni na kuwasihi wanafunzi kuwa na nidhamu kwa walimu na jamii yote kwa ujumla.


Akiongea kwa niaba ya wanafunzi waliopokea baiskeli hizo, Claudia Njijila mwanafunzi wa shule ya Sekondari Banyibanyi amesema awali walipata shida ya kutembea umbali mrefu jambo lililopelekea wao kuchoka na kushindwa kusoma vizuri lakini baiskeli zitawasaidia kuwahi shule na kupata muda mzuri wa kujisomea.


Kwa upande wao wazazi wa wanafunzi hao wamesema kuwa awali walipata adha kubwa na walitakiwa kudamka saa 10 usiku ili kuwasindikiza watoto wao kwenda shule, hivyo wanashukuru Wahandisi wasio na Mipaka kutoka Marekani kwa msaada huo.


Akiongea kuwakilisha jumuiya ya Shule,Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mkutani, Samwel Chidabile amesema anashukuru Wahandisi wasio na Mipaka kwani wamekuwa ni marafiki bora tangu mwaka 2017 walipofanya shughuli za kuboresha miundombinu ya shule hiyo na mpaka sasa wamepokea baiskeli 121 ambazo zinasimamiwa na kamati ya shule kuhakikisha zinakuwa salama na kutumika kwa wanafunzi.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.