• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

WAHITIMU VETA KUPEWA KIPAUMBELE KATIKA SHUGHULI ZA MIRADI YA SERIKALI

Imewekwa: June 24th, 2025

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa na Diwani wa Kata ya Kongwa Mhe. White Zuberi amewaahidi wanachuo wa Chuo cha Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA) Kongwa kuwa watapatiwa fursa ya kushiriki katika ujenzi wa majengo yote ya karibu yanayojengwa na Halmashauri ili kuwawezesha kufanya mafunzo yao kwa vitendo.

Mhe. Zuberi ameyasema hayo alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya pili ya fani ya uhazili na kompyuta katika Chuo cha Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA) Kongwa ambapo ameeleza kuwa wanachuo hao watashiriki kufanya mafunzo kwa vitendo katika majengo ya Serikali ili watakapomaliza chuo wawe mafundi bora na mahiri.

Vilevile Mhe. Zuberi amewatia moyo wahitimu na kuwasihi waone fahari juu ya ujuzi walioupata kwani una tija kwa jamii na utawawezesha kujiajiri na kupata elimu ya juu zaidi hivyo watumie ujuzi huo kwa kuanzisha vikundi, kubuni miradi ya maendeleo na kuunda vikundi vya vijana ambavyo Halmashauri itavipatia fedha za 10% kwaajili ya kuendesha miradi.

Aidha Mhe. Zuberi amefafanua kuwa kwa changamoto ya upatikanaji wa leseni za usafiri, Halmashauri itawasiliana na ofisi ya mapato TRA ili waweze kuweka mfumo rahisi wa utoaji leseni ndani ya Wilaya ili wanachuo hao wanapomaliza mafunzo yao waweze kupata leseni hizo kiurahisi bila kwenda Mkoani.

Mgeni rasmi katika mahafali Mhe. White Zuberi akitoa neno kwa wahitimu

Mkuu wa chuo cha VETA Kongwa Bwana Abdulkadir Yusuff ameshukuru Serikali kwa kuwapatia vifaa katika fani za uhazili, kompyuta, ushonaji na uwashi na kukiri kuwa kupitia chuo hicho wafanyabiashara watanufaika kwa kuuza vifaa vya ufundi na wananchi kupata huduma bora na rahisi kupitia wahitimu wa chuo hicho.

Licha kutaja changamoto za ukosefu wa vifaa katika fani za useremala na ufundi magari, upungufu wa mashine za kuchapa, upungufu wa vitendea kazi katika karakana na ofisi za walimu, ukosefu wa karakana ya uhazili na kompyuta, upungufu wa mabweni lakini Mwl. Yusuph amesema kuwa chuo kinaendelea kutekeleza wajibu wake wa kutoa mafunzo.

Mkuu wa chuo cha VETA  Kongwa akiongea wakati wa mahafali hayo

Kwa upande wao wahitimu hao 11 wameshukuru na kupongeza Serikali ya awamu ya sita, uongozi wa chuo pamoja na wakufunzi wao kwa elimu waliyoipata na kueleza kuwa wamefanikiwa kupata ujuzi mahiri wa nadharia na vitendo utakaowawezesha kufanya kazi maeneo mbalimbali hivyo wapo tayari kutumikia Taifa kwa ujuzi waliopata.

Aidha katika Risala yao wahitimu hao wameomba Serikali kujenga maktaba yenye vitabu vya kujifunzia, na kuomba kila muhitimu kupewa vifaa vya kuanzia kufanya kazi kulingana na fani yake ili kujenga dhana kamili ya kujiajiri.

Wahitimu wakisoma risala mbele ya mgeni rasmi.

Baadhi ya fani zinazotolewa katika Chuo cha mafunzo ya Ufundi stadi VETA Kongwa chenye jumla ya wanafunzi 245 ni pamoja na uhazili na kompyuta, umeme wa magari majumbani na viwandani, ujenzi, uwashi, seremala, udereva wa magari na pikipiki na fani ya ushonaji.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI WALA KIAPO.

    August 04, 2025
  • DED KONGWA AKABIDHI TAA 390 KWA WATUMISHI WA AFYA

    July 28, 2025
  • ECOKAZI WATOA MAFUNZO KUHUSU BIASHARA YA KABONI

    July 24, 2025
  • WASIMAMIZI WA AFYA WANOLEWA UDHIBITI NA UTENGANISHAJI TAZIHA.

    July 23, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.