• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Wakulima na Wafanyabiashara wa Mazao Epukani Ufungashaji wa Lumbesa

Imewekwa: June 28th, 2018

Serikali kupitia Wakala wa Vipimo Tanzania Bara, inaendelea kuwasisitiza Wakulima na Wafanyabiashara wa mazao kuepuka ufungashaji wa lumbesa na kutumia vipimo halali kutokana na madhara Mengi yatokanayo na ufungashaji huo pamoja na kuhakikisha wanatumia mizani ambayo haijaharibika.

Afisa wa Wakala wa Vipimo Tanzania Bara, Mkoa wa Dodoma Bw. Saidi Ibrahim June 27, 2018 amewaeleza Wajumbe wa Baraza la Biashara la Wilaya ya Kongwa kuwa kazi kubwa inayofanywa na Taasisi ya Wakala wa Vipimo Tanzania ni kusimamia matumizi sahihi ya Vipimo vya aina zote ili ikiwemo vipimo vya ujazo, uzito na urefu na kupiga marufuku Vipimo batili, yaani visivyo na ulinganifu.

Bw. Ibrahim amesema ufungashaji wa Lumbesa ni Ukiukwaji wa Taratibu za Vipimo na ameyataja madhara ya Lumbesa ni pamoja na kumpunja mkulima kutokana na ujazo huo kuzidi ujazo wa gunia la kawaida, hivyo mkulima hulazimika kuuza Lumbesa kwa bei ya ujazo wa kawaida.

Madhara mengine ni ya Kiafya kwa wabebaji, kutumia nguvu nyingi kupita uwezo wao na kutokuwa na uwiano kati ya Kilo za mbebaji na mizigo iliyofungashwa kwa mfumo huo wa Lumbesa, pia, huharibu miundombinu na kuharibu vyombo vya usafiri.

“Aidha, Lumbesa hudhoofisha ukusanyaji wa mapato, kwani mwenye mazao anapotozwa tozo kwa gunia moja huku amefungasha lumbesa ni dhahiri ufungashaji wa Lumbesa hupita vipimo halisia”. Amesisitiza Bw. Ibrahim.

Dinah Mlay ni mmoja wa Wafanyabiashara watumiao mizani ambaye pia ni mjumbe wa Baraza la Biashara kupitia Sekta Binafsi amesema, “kumekuwa na Changamoto za gharama kubwa za mafundi warekebisha mizani ambapo gharama hizo huzidi gharama ya manunuzi ya mzani mpya, hivyo anaomba Taasisi hiyo kuliangalia suala hilo kwa undani”. Aidha, Ibrahim alisema Faida ya Vipimo halisia vinakuza uchumi binafsi na uchumi wa Taifa, na kusaidia katika soko la ushindani ndani na nje ya nchi.

Ambapo Bw. Ibrahim amesema amelipokea na sehemu husika. Aidha,Sheria ya Vipimo inataka Vipimo vyote ikiwemo mizani, pampu za mafuta kukaguliwa na maafisa vipimo Mara moja kwa kila mwaka. Hivyo, Mlaji asipofanya hivyo, atakuwa amevunja sheria ya Vipimo

Pia, Bw. Ibrahim amesema Faida ya Vipimo halisia vinakuza uchumi binafsi na uchumi wa Taifa, na kusaidia katika soko la ushindani ndani na nje ya nchi.

Mwishowe, Wajumbe wa Baraza wakapata mafunzo ya Vitu muhimu vya kuzingatia katika Ufungashaji wa mvuto wa bidhaa mbalimbali, ambapo Bw. Ibrahim alibainisha kuwa ni kuhakikisha Bidhaa inakuwa na Jina, mahali inapotengenezwa, Jina la msambazaji, Anuani ya Posta, Barua pepe, Simu, Kiasi halisi cha Vipimo cha bidhaa, lugha inayotafsirika mahali inapoenda kuuzwa.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.