• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

WALIMU WAKABIDHIWA NYUMBA ZILIZOJENGWA NA MFUKO WA MAENDELEO TASAF

Imewekwa: February 28th, 2025

Walimu wanufaika wa nyumba zilizojengwa na mfuko wa maendeleo ya Jamii Tasaf wameaswa kuzitunza nyumba hizo na kuhakikisha zinakuwa katika mazingira mazuri na nadhifu ili mradi huo uwe wenye tija katika shule ya sekondari Chitego.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Omary Nkullo katika hafla ya kukabidhi nyumba za walimu katika Kata ya Chitego. Dkt Nkullo pia amempongeza na kumshukuru mbunge wa jimbo la Kongwa Mhe. Job Ndugai kwa kuhakikisha anapambana usiku na mchana ili majengo hayo yanajengwa katika Kata ya Chitego. Pia ameshukuru diwani na timu yake pamoja na watendaji wa kata na vijiji kwa kujitoa kwa dhati kuhakikisha ujenzi wa nyumba hizo unakamilika.

Kabla ya kukabidhi kipaza sauti, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ameeleza kuwa sababu Serikali inatoa fedha nyingi kujenga miradi ya elimu ikiwemo nyumba za walimu na wananchi wamekuwa wakitumia nguvu zao kuhakikisha miradi husika inakamilika, hivyo wananchi hawana budi kuhakikisha kuwa wanahamasisha wanafunzi kutumia fursa za elimu na kujiandikisha na kuhakikisha wanasoma ipasavyo kwani hakuna urithi mwingine wa kumwachia mtoto ila elimu.

Akiongea kabla ya kukabidhi vyeti, Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tasaf Ndg. Salum Mshana ameeleza furaha yake baada ya kukagua mradi na kudai kuwa ukamilishaji umefanyika kwa usahihi na Tasaf ikiwakilishwa na yeye mwenyewe imefurahi kwa mradi kuisha kwa wakati na kwa viwango vinavyostahili.

Akihitimisha ndg. Salum Mshana amefafanua kuwa mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tasaf uko nchi nzima na amewasifu viongozi kwa kupambana kuhakikisha majengo hayo yanajengwa Chitego na yanakamilishwa kwa ukamilifu wake.

Naye Mbunge wa jimbo la Kongwa na Spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai ameeleza furaha yake kuona mradi huo umekamilika na umefikia kukabidhiwa kwa wanufaika. Pia amepeleka shukrani zake za dhati kwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwa mradi huo umefanyika chini ya serikali yake.

Akiongea baada ya kupokea nyumba, Mwalimu wa shule ya sekondari Chitego mwl. Ramadhani Hamza ameeleza furaha yake kukabidhiwa nyumba na ametoa shukrani zake za dhati kwa uongozi wa Wilaya, Kata na Kijiji kwa kuhakikisha mradi huo unakamilika bila kusahau uongozi wa Tasaf ambao wametoa fedha za mradi. Mwl. Ramadhan ameeleza kuwa majengo hayo yanaenda kurahisisha ufanyaji kazi wa walimu muda wowote ikiwemo muda wa usiku lakini pia nyumba hizo zinaenda kuwapunguzia walimu umbali wa kutoka nyumbani Kwenda shule kufundisha.

Naye kiranja mkuu wa shule ya sekondari chitego Goodluck Frank ameeleza furaha yake kuona walimu wake wakipatiwa nyumba hizo karibu na shule na kudai kuwa itarahisisha walimu kuwasaidia wanafunzi muda wa maandalizi ya kujisomea baada ya muda wa kawaida wa  shule kuisha kwani changamoto waliyokuwa nayo ilikuwa kupata usaidizi baada ya masomo kuisha na wakati wanajisomea. Pia ameonyesha Imani yake kuwa ufaulu utaongezeka kutokana na uwepo wa majengo hayo kwani wanafunzi wakiwa katika masomo ya usiku watapata usimamizi na usaidizi wa walimu ambao wako karibu na shule.

Aidha Mratib wa Tasaf Wilaya ya Kongwa ndugu. Elias Chilemu ameeleza kuwa takribani shilingi za kitanzania milioni mia moja themanini na nane zimetumika kukamilisha mradi huo na kumshukuru Mhe. Mbunge kwa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha upatikanaji wa fedha hizo kwa ajili ya mradi. Ndg. Chilemu ametoa rai kwa majengo hayo kuleta tija katika ufaulu wa wanafunzi kwani dhumuni la Tasaf kushiriki katika kuhakikisha mradi huo unakamilika ni ili walimu waweze kuwa na ukaribu na wanafunzi wao kuwasaidia katika muda wa ziada wa masomo ili ufaulu uongezeke.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.