• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

’Wanafunzi wa Madarasa ya Mitihani wapunguziwe shughuli za nyumbani’’ RC Mtaka.

Imewekwa: May 8th, 2022

Na Stephen Jackson

KONGWA.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka amewataka wazazi wenye wanafunzi waliopo kwenye madarasa ya mitihani ya Taifa, kuwapunguzia kazi za nyumbani ili kuwapa muda zaidi wa kujisomea.

Mhe. Antony Mtaka ameyasema hayo leo Jumapili Tarehe 08 Mei, 2022 wakati akihutubia waumini wa kanisa la Anglikana Kongwa Dayosisi ya Mpwapwa, katika ibada Maalumu iliyoendeshwa na Askofu wa Dayosisi hiyo Mhashamu Dr. Jacob Erasto Chimeledya. ‘’ Wazazi wote ambao wana watoto waliopo kwenye mitihani ya taifa mwaka huu, shule ya msingi mtihani wa Taifa ni Darasa la nne na darasa la saba. Kidato cha kwanza mpaka cha nne ni "form II" na "Form Four". Wazazi wote ambao wana watoto waliopo kwenye madarasa ya Mitihani ya Taifa wawapunguzie shughuli za nyumbani, watoto wapate  muda mzuri wa kufanya maandalizi ya kujisomea.’’ Alitanabaisha Mheshimiwa Mtaka.

Sanjali na hayo Mhe. Mtaka ameziagiza kamati za shule pamoja na wazazi kukutana na kutafuta namna watakavyoweza kuwasaidia watoto hao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanapata chakula Cha mchana shuleni,  lengo likiwa ni kuwapa muda zaidi wa kujisomea.

Mheshimiwa Mtaka alizungumza hayo kufuatia matokeo yasiyoridhisha Wilayani Kongwa ambapo alibainisha kuwa Mbunge wa Jimbo la Kongwa na Spika Mstaafu Mhe. Job Yustino Ndugai anaendelea na ufuatiliaji kuhusu changamoto hiyo.

Katika ibada hiyo Mhe. Mtaka amechangia jumla ya mifuko 100 ya saruji kwaajili ya ujenzi wa ofisi za kanisa hilo pamoja na madirisha sita ya ‘’Alminium’’ kwaajili ya umaliziaji wa jengo la Kanisa hilo la Mtakatifu Michael, Dayosisi ya Mpwapwa.

Ili kufanikisha ujenzi wa kanisa hilo ambalo lipo katika hatua ya umaliziaji , Mheshimiwa Mtaka ameendesha harambee ya kuchangia ujenzi huo unaoendelea kwa viongozi wa chama na serikali walioshiriki ibada hiyo na kufanikisha kupatikana kwa saruji na Madirisha ya vioo.

Kwa upande wake Askofu Jacob Chimeledya kupitia Mahubiri ya ibada hiyo, ametoa wito kwa viongozi wa Serikali  ya Tanzania kutokukiri kwa wananchi  kuwa nchi yetu ni Nchi maskini kwa kuwa  inazo raslimali za kutosha. ‘’Inchi yetu Ina Mali nyingi, hakuna sababu wala haiko sababu ya viongozi wetu wa Tanzania kukiri kwamba sisi tuko Maskini.’’  Alisema Askofu Chimeledya.

Katika Ibada hiyo akinamama wa kanisa hilo wakiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Dr. Faith Mganga walikabidhi gari aina ya ‘’Toyota Noah’’ lenye namba za usajili T479 DZD kwa Mchungaji wa kanisa hilo kwaajili ya huduma za kanisa.  Kwa mujibu wa Mwakilishi wa Kampuni ya Fahari Motors waliofanikisha uagizaji wa gari hilo ametaja thamani ya gari hilo kuwa ni Tshs. 19,500,000/=.

Taarifa ya Akinamama hao, inaeleza kuwa fedha za ununuzi wa gari hilo zimetokana  na michango yao wenyewe pamoja na wadau mbalimbali, akiwemo Mkuu wa wilaya ya Kongwa Mheshimiwa Remidius Mwema Emmanuel chini ya usimamizi wa Dr. Faith Mganga, Muumini na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma.

 

 

Matangazo

  • Kuitwa kwenye Usaili Ajira za muda -TASAF December 02, 2022
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2022 December 01, 2022
  • Kuitwa kazini Ajira za Muda - TASAF December 06, 2022
  • Fomu ya Maelekezo ya kujiunga na shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa. May 18, 2022
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • Viongozi wa kisasa watakiwa kushirikiana na wataalamu

    March 12, 2023
  • Watendaji wote waahidiwa kupewa pikipiki

    February 17, 2023
  • Kongwa kumalizia tatizo la Upimaji Ardhi.

    February 14, 2023
  • Mkurugenzi Kongwa aonya wazazi wanaokatisha tamaa wanafunzi.

    February 13, 2023
  • Tazama Yote

Video

''KONGWA MMEUPIGA MWINGI''
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)
  • Bunge la Tanzania

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 737 798 222

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.