• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Wanaoharibu Miundombinu ya Maji kukiona

Imewekwa: September 27th, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Meneja wa RUWASA (Wakala wa maji vijiji na Usafi wa mazingira) Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma  mhandisi Kaitaba Rugakingira, ameonya tabia ya uharibifu wa miundombinu ya maji unaofanywa na watu wasio waaminifu katika maeneo mbalimbali.

Rai hiyo imetolewa tarehe 27 Septemba, 2022 wakati akihitimisha semina ya siku mbili kwa wajumbe wa vyombo vya watumia maji ngazi ya jamii, iliyofanyika ukumbi wa VETA Kongwa ikihusisha kata mbili za Ugogoni na Mtanana zinazonufaika na mradi wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi, unaotekelezwa na Shirika la "Foundation for Energy, Climate and Environment" (FECE)

Mhandisi Rugakingira ameeleza kuwa uharibifu wa miundombinu hupelekea matengenezo ya mara kwa mara, hivyo amewaagiza wajumbe wa kamati hizo kuhakukisha wanailinda miundombinu ya maji katika maeneo yao.

Aidha ameongeza kuwa yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria Ikiwa ni pamoja na kulipa faini kati ya shilingi milioni Moja hadi milioni tano.

Mhandisi Rugakingira, amezishauri kamati za usimamizi wa maji kufunga mita maalumu (bulk meter) kwenye matenki ya maji Ili kubaini kiasi halisi cha maji kinachosambazwa kwa watumiaji.

Naye mtaalamu wa elimu ya jinsia na  mkufunzi wa semina hiyo ndugu Emmanuel Mroto kutoka kituo cha jinsia SUA, ameeleza kuwa kwa muda mrefu mahitaji ya wanawake yamekuwa hayapewi kipaumbele katika utekelezaji wa miradi ya jamii hivyo Kuna Kila sababu  ya kuijengea uwezo jamii.

Akichangia hoja katika semina hiyo, Samson Lazaro Daudi mkazi Kata ya Mtanana, amewataka viongozi wa vijiji kutekeleza majukumu yao kwa weledi Ili kuzuia migogoro ya ardhi na uharibifu wa Mazingira vikiwemo vyanzo vya maji.

Kwa upande wake Remmy Malogo Mwenyekiti wa chombo cha watumia maji Kijiji cha Ibwaga pamoja na kukiri kunufaika na semina hiyo, pia ameshauri kuwepo kwa tathmini endelevu ya utendaji kazi Ili kubaini tija ya mafunzo hayo.

Kwa upande wao Mafundi wa miradi ya maji Sospeter Mkoma wa Chigwingwili na Bahath Packshard wa Mtanana "B" wametoa shukurani  kwa RUWASA na FECE kwa kuwapatia mafunzo hayo ambayo yamewajengea uwezo wa kukabiliana na changamoto kadha wa kadha.

Mafunzo haya ya kuwajengea uwezo wajumbe wa vyombo vya watumia maji, yamewanufaisha washiriki kwa kuwafunulia mbinu na maarifa  mapya juu ya usimamizi wa miradi ya maji na utunzaji wa Mazingira.

Katika semina hiyo kamati hizo zimeshauriwa mbinu mbalimbali za kuziba mianya ya upotevu wa maji na mapato ikiwemo kuwaelimisha wananchi, na kuhamasisha matumizi ya mita za kisasa za malipo ya Kabla ya bili za

maji (LUKU), ambapo mteja hulipa huduma ya maji kadiri anavyotumia.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.