• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

WASIMAMIZI WA AFYA WANOLEWA UDHIBITI NA UTENGANISHAJI TAZIHA.

Imewekwa: July 23rd, 2025


Na Bernadetha Mwakilabi

Habari – Kongwa DC

Wasimamizi wa huduma za afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa wamepatiwa mafunzo ya udhibiti na utenganishaji takataka zitokanazo na huduma za Afya (TAZIHA) kwa kusudi la kuwajengea uwezo wa kusimamia taka hizo ili zisiweze kuleta athari za kimazingira na kiafya.

Mafunzo hayo yametolewa mwishoni mwa juma lililopita ikiwa ni sehemu ya kutekeleza agizo la Mkurugenzi Mtendaji wa Ustawi wa Jamii na Lishe Tamisemi Dkt. Rashid Mfaume alipotembelea Wilaya ya Kongwa ambapo aliagiza kutolewa mafunzo hayo kutokana na changamoto alizozibaini za usimamizi hafifu wa TAZIHA na matumizi ya maji safi na usafi wa mazingira.

Nae Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Dkt. Thomas Mchomvu wakati akifunga mafunzo hayo licha ya kuagiza vituo vya afya kununua vifaa vya kufanyia usafi lakini pia amewataka watumishi wa afya wote kusoma mara kwa mara miongozo ya Wizara ya afya ili iwasaidie katika utendaji kazi wao kwa kulinda afya na mazingira pamoja na kufanya ajenda ya usimamizi wa taka na unawaji mikono kuwa ya kudumu katika kila kikao.

Dkt. Mchomvu ameeleza kuwa ukusanyaji, utenganishaji na usafirishaji wa Taziha ni changamoto katika vituo vya kutolea huduma za afya Wilayani Kongwa kutokana na watumishi wengi waliokuwa na uzoefu wa usimamizi huo kustaafu na waliopo kazini asilimia kubwa kuwa ni wageni walioajiriwa miaka ya karibuni.

Nae Bw. Nelson Rumbeli, Afisa Afya Mkoa wa Dodoma na mkufunzi katika mafunzo hayo ameeleza kuwa kumekuwa na ongezeko la utoaji huduma katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini, jambo linalopelekea kuwepo kwa uzalishwaji wa taka kwa kiasi kikubwa hivyo ni vyema watumishi watambue namna ya kuzitunza taka hizo ili zisilete athari.

Vilevile Bw. Rumbeli ameongeza kuwa kumekuwa na changamoto katika vituo vya afya zinazopelekea ugumu katika utenganishaji wa taka hizo ikiwemo uelewa mdogo na usimamizi hafifu wa taka katika vituo, kutokuwepo kamati za kusimamia utenganishaji taziha, vituo vya afya kutokuwa na mizani ya kupimia taziha pamoja na vituo vya afya kutokuwa na takwimu za Taziha.

Pamoja na hayo, Afisa Afya Wilaya ya Kongwa Bw. Mdasilu Bashiru amesema kuwa usimamizi wa Taziha unakabiliwa na changamoto ya usimamizi hafifu wa taka, kutokuwepo kwa takwimu sahihi za ukusanyaji taka na uhaba wa vichomea taka ambapo katika vituo vya kutolea huduma za afya 72 ni vituo vya afya 6 na zahanati 6 zenye vichomea taka vya kisasa.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • ECOKAZI WATOA MAFUNZO KUHUSU BIASHARA YA KABONI

    July 24, 2025
  • WASIMAMIZI WA AFYA WANOLEWA UDHIBITI NA UTENGANISHAJI TAZIHA.

    July 23, 2025
  • MWENYEKITI KIJIJI CHA MLANJE ARUDISHWA MADARAKANI.

    July 21, 2025
  • DED KONGWA APONGWEZWA UTOAJI MIKOPO 10%.

    July 18, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.