• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

WATAFITI KUTOKA CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA KILIMO (SUA) KUTAMBULISHA MRADI WA UTAFITI WA MNYOO TEGU WA NGURUWE (NEUROSOLVE PROJECT) WILAYANI KONGWA.

Imewekwa: October 3rd, 2024


Kongwa, Dodoma.

Watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) wametambulisha mradi wa utafiti wa mnyoo tegu wa nguruwe ujulikanao kwa jina la ‘neurosolve project’ katika kikao na wajumbe wa Halmashauri ya wilaya ya Kongwa. Baada ya kuwatambulisha wajumbe wa Halmashauri, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa dkt. Omary Nkullo akamkaribisha Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. White Zuberi Mwanzalila ambaye alitumia wasaa huo kufungua kikao rasmi.

Akitoa elimu kwa niaba ya watafiti waliohudhuria katika kikao hicho, Dkt. Ernatus Mkupasi, Mtafiti na Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo ameelimisha wajumbe wa Halmashauri kwa kuelezea mzunguko mzima wa kusambaa kwa mnyoo tegu kati ya binadamu na nguruwe.


Dr. Ernatus Mkupasi, Mtafiti na Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) akitoa elimu kwa wajumbe wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.

Dkt Ernatus Mkupasi ameeleza mzunguko wa mnyoo tegu kutoka kwa binadamu Kwenda kwa nguruwe na kutoka kwa nguruwe Kwenda kwa binadamu na ameanza kwa kueleza kuwa mnyoo tegu akiwa tumboni kwa binadamu,huishi katika utumbo mwembamba na anaweza kukuwa kwa urefu wa mita sita mpaka kumi, mnyoo huyo akishakomaa huwa anaachia pingili zilizopo kwenye sehemu ya mkia wake, watafiti wamebaini kuwa pingili moja hubeba mayai takribani elfu Hamsini. Pingili hizo hutoka katika utumbo wa binadamu kwa njia ya haja kubwa. Tabia hatarishi za binadamu ikiwemo kujisaidia katika vyanzo vya maji ama maeneo yasiyo rasmi kutumika kama vyoo husababisha kusambaa kwa mayai haya kwenda kwa nguruwe kwa njia mbalimbali. Mfano nguruwe akitumia maji yenye mayai ya mnyoo tegu ama nguruwe akilishwa chakula chenye mayai ya mnyoo huyo. Mayai yaliyoingia katika mwili wa nguruwe huanguliwa na kusambaa sehemu mbalimbali ya mwili wa nguruwe. Nguruwe mwenye mnyoo tegu husambaza mnyoo huo kwa binadamu endapo nyama yake yenye mnyoo tegu italiwa na binadamu.


Mchoro wa usambazwaji wa mayai ya mnyoo Tegu kati ya binadamu na nguruwe.

Mtafiti ameeleza kuwa binadamu mwenye mnyoo Tegu anaweza kusambaza mayai ya mnyoo huyo kwa binadamu mwingine endapo hatazingatia usafi wa kina baada ya kutumia choo na kushikana mikono na binadamu mwingine ambaye kwa namna moja ama nyingine atameza mayai hayo kwa kula chakula bila kusafisha mikono yake. Pia unywaji wa maji yasiyo safi na salama yenye mayai ya mnyoo tegu ni njia mojawapo ya binadamu kumeza mayai ya mnyoo huyo na endapo mayai hayo yataingia mwilini mwa binadamu basi yataanguliwa na ukuwaji wa mnyoo tegu utaendelea katika mwili wa binadamu.



Aidha Dkt Ernatus Mkupasi ameainisha changamoto mbalimbali ambazo zinaweza kumpata binadamu pindi atakapopata mnyoo wa aina hii na kueleza kuwa binadamu akipata mnyoo Tegu na kukaa kwenye mfumo wa fahamu basi anawezapata changamoto mbalimbali ikiwemo Kupoteza kumbukumbu, Maumivu ya kichwa yasiyoisha,Changamoto za Kifafa, Kupooza na matatizo mengine ya afya ya akili ikiwemo kichaa.

Changamoto nyingine ambazo binadamu anawezakukumbana nazo ni changamoto za kiuchumi ambazo zitaletwa na gharama za matibabu pindi binadamu atakapogundulika kuwa na mnyoo Tegu, lakini pia uharibifu wa nyama na mifugo ambayo imeathiriwa na mnyoo tegu sababu nyama hiyo inakuwa sio salama kutumika tena kwa binadamu.

Akiongea wakati wa kufunga kikao, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhe. White Zuberi ameshukuru watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa elimu iliyotolewa na kuhimiza mchakato huu wa elimu kupitia wataalamu na wajumbe mbalimbali wa Halmashauri uwafikie wananchi ili wapate ufahamu wa changamoto hii ya mnyoo Tegu.


Washiriki katika kikao cha uzinduzi wa Mradi wa mnyoo Tegu wa nguruwe (neurosolve project) wakiwa katika picha ya pamoja.

Uzinduzi wa mradi huu ni muendelezo wa jitihada za dhati zinazofanywa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kwa kushirikiana na serikali Pamoja na vyuo vingine vilivyopo ndani na nje ya nchi, pamoja na wadau wengine wa afya ikiwemo Umoja wa Ulaya ili kutokomeza changamoto hii ya mnyoo Tegu wa nguruwe. Mradi huu pia unalenga  kuendelea kutoa elimu endelevu juu ya changamoto hii ambapo elimu hii itagusa maeneo mbalimbali ikiwemo mazingira kwa kuhamasisha usafi wa mazingira na matumizi ya vyoo  kwa baadhi ya watu wasiotumia vyoo, lakini pia maeneo mengine kama afya ya mifugo ikihusisha ukaguzi wa nyama kabla haijamfikia mlaji.

Imeandaliwa na;

MASHA E. MBONEA

K/MKUU KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI WILAYA YA KONGWA.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.