• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Watanzania watakiwa kutambua na kuthamini historia ya Wapigania Uhuru katika Eneo la Kongwa

Imewekwa: April 3rd, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emmanuel, amewataka Wakazi wa Wilaya ya Kongwa na Watanzania kwa ujumla kutambua na kuthamini historia ya Eneo hilo ambalo lilitumika katika harakati za Ukombozi wa nchi za Kusini Mwa Afrika.

Mhe. Emmanuel alisema hayo wakati akiwa mbioni kuhitimisha ziara ya Mabalozi kutoka nchi tano (5) za Kusini Mwa Afrika hapa nchini Tarehe 02/04/2021.

Aidha Mhe. Mwema ameongeza kuwa, endapo wananchi watathamini historia ya harakati za wapigania Uhuru katika eneo hilo la Kongwa, kitendo hicho kitayapa nguvu Mataifa mengine pia.

"Tunaona Ni heshima kubwa ya  kuwa sehemu ya historia ya Nchi za Kusini Mwa Afrika na tungetamani mataifa yote hayo yaweze kutambua hili" Alisema Mhe. Emmanuel.

Akizungumza katika kikao maalumu kilichofanyika katika ukumbi wa shule ya Sekondari Kongwa Balozi wa Namibia hapa nchini, Mhe. Lebbius Tangeni Tobias, alisema, Kongwa ni sehemu ya pekee kwa kuwa Viongozi wengi waliopigania Uhuru wa Nchi za Kusini Mwa Afrika waliweza kuishi, huku wengine wakipoteza Maisha katika eneo hili. 

Naye Balozi wa Msumbiji hapa nchini Mhe. Ricardo Mtumbuida   alieleza kuwa Lengo la ziara ya timu  hiyo ya Mabalozi  ni kujionea halihalisi ya Miundombinu ya kambi ya Wapigania uhuru ili waweze kushirikiana na serikali ya Tanzania hususani Wilaya ya Kongwa kufanya  ukarabati wa Majengo kambini hapo  kwa Lengo la kutunza historia ya Eneo hilo kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Balozi Mtumbuida, ameongeza kuwa Eneo la Kongwa ni miongoni Mwa Maeneo muhimu ya Ukombozi wa Nchi za Kusini Mwa Afrika kupitia  hamasa au jitihada za Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere aliyeamini kuwa Tanzania haiwezi kuwa huru mpaka hapo Afrika yote itakapokuwa huru.

Katika ziara hiyo, Mabalozi na Viongozi mbalimbali walipanda miti ya kumbukumbu na kutembelea Maeneo mbalimbali ya kihistoria.

Mabalozi wengine waliokuwepo kwenye ziara hiyo ni Balozi wa Angola Bwana.Sandro De Oliveira, Balozi wa Zimbabwe Lt. Gen. Anselem Senyatwe na Bi. Stella V. Dhlomo kutoka Afrika ya Kusini aliyeambatana na Kanali Bongani Majola.

Kambi ya Wapigania uhuru wa Nchi za Kusini Mwa Afrika iliyopo Wilayani Kongwa, inahusisha Mataifa ya Angola, Msumbiji, Zimbabwe, Afrika ya Kusini, na Namibia.



Matangazo

  • Kuitwa kwenye Usaili Ajira za muda -TASAF December 02, 2022
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2022 December 01, 2022
  • Kuitwa kazini Ajira za Muda - TASAF December 06, 2022
  • Fomu ya Maelekezo ya kujiunga na shule ya Sekondari ya Wasichana Kibaigwa. May 18, 2022
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • Viongozi wa kisasa watakiwa kushirikiana na wataalamu

    March 12, 2023
  • Watendaji wote waahidiwa kupewa pikipiki

    February 17, 2023
  • Kongwa kumalizia tatizo la Upimaji Ardhi.

    February 14, 2023
  • Mkurugenzi Kongwa aonya wazazi wanaokatisha tamaa wanafunzi.

    February 13, 2023
  • Tazama Yote

Video

''KONGWA MMEUPIGA MWINGI''
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)
  • Bunge la Tanzania

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 737 798 222

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.