• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Watendaji vijiji wa kujitolea wahimizwa uzalendo

Imewekwa: September 5th, 2022

Na Stephen Jackson, Kongwa.

Watendaji vijiji wanaojitolea katika maeneo mbalimbali wilayani Kongwa, wametakiwa  kudumisha uzalendo licha ya kukosa  nafasi za ajira za kudumu kupitia zoezi la usaili lililohitimishwa Jumapili ya tarehe 4, Septemba 2022.

Salamu hizo zimetolewa na wajumbe mbalimbali wa kikao Cha kamati ya fedha Wilaya ya Kongwa kilichoketi Septemba 5, 2022 chini ya Mwenyekiti wake Mhe. White Zuberi Mwanzalila.

Mhe. White Zuberi Mwanzalila ameieleza kamati kuwa zoezi hilo limekwenda vizuri Kwa kusimamiwa kikamilifu kwa mujibu wa Sheria, taratibu na kanuni ambapo bodi ya Ajira, sekretarieti ya Ajira pamoja na Idara ya utumishi na Utawala walihakikisha haki inatendeka Ili kupata waajiriwa wenye sifa.

Akichangia hoja kwenye taarifa ya Idara ya utumishi na Utawala Diwani wa Kata ya Iduo Mhe. Valentino Seng'unda  ameeleza kuwa kutokana na watendaji wa vijiji wa kujitolea kukosa nafasi za ajira za kudumu, ipo haja ya kufanyika vikao rasmi vya makabidhiano kwenye Ofisi zilizo kaimishwa ili kunusuru usalama wa nyaraka kutokana na hisia hasi kwa baadhi ya watendaji waliokosa nafasi za ajira.

 "Kwa hasira yao ya kukosa nafasi ya kuwa Watumishi wa Serikali, kutokana na nafasi walizozikosa yawezekana kuna taarifa nyingi zitapotea kwenye eneo lile husika. Sasa ninachoomba kwa kuwa Idara  ya utumishi kwa kuwa imeshapata wale wanaotakiwa kuwa na nafasi za utendaji kamili iwe na vikao rasmi vya makabidhiano" Alieleza Mhe. Seng'unda.

Akijibu hoja hiyo, Mkuu wa Idara ya  Utawala na Utumishi ndugu Fortunatus Mabula amewataka Watumishi hao wa  kujitolea kutokata tamaa kwani suala la kukosa ajira hizo siyo mwisho wa maisha na hivyo ametoa wito Maalumu Kwa watendaji hao kufika ofisini kwa ajili ya majadiliano.

 "Nimewaomba waje ofisini kwangu waje tujadiliane, wasifikiri ndiyo mwisho wa maisha".  Alinukuliwa Ndugu Mabula.

Aidha katika mchakato wa usaili waombaji wa nafasi hizo walipongeza mchakato mzima wa usaili kwa kuzingatia Misingi ya haki na utu.

Kupitia usaili huo jumla ya nafasi 34 za Watendaji wa Vijiji Daraja la III zimejazwa ambapo pindi Watumishi hao wapya watakapo ripoti na kupangiwa vituo vya kazi, hatua hiyo itasitisha mikataba ya watendaji wa kujitolea.

Kikao hicho cha kisheria cha kamati ya Fedha kiliketi kupokea na kujadili taarifa mbalimbali za fedha.

 

Mhe. White Zuberi Mwanzalila- Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.

Dkt. Omary Nkullo - Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.

Mhe. Valentino Seng'unda - Diwani wa Kata ya Iduo

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

    April 25, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.