• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

WAUGUZI WAASWA KUZINGATIA MAADILI KATIKA KAZI

Imewekwa: June 19th, 2025

Wito umetolewa kwa wauguzi kuwajibika kwa kuwa na maadili mema, kutoa huduma bora kwa wateja wao na kuhakikisha wanasimamia matumizi sahihi ya vitendea kazi ili kuzuia vitendo vitakavyoharibu tasnia ya uuguzi.

Wito huo umetolewa na Afisa Elimu sekondari Wilaya ya Kongwa Ndugu Sudy Abdul alipomuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kongwa katika maadhimisho ya Siku ya wauguzi Duniani katika viwanja vya Hospitali ya Wilaya ya Kongwa ambapo amesisitiza wauguzi kuepuka mianya ya upotevu wa mapato pamoja na vifo vya watoto wachanga na akina mama wanaojifungua.

Mgeni rasmi Mwl. Sudy Abdul akitoa nasaha zake kwenye hafla.

Licha ya kuwapongeza wauguzi, Ndg. Sudi Abdul amesema kuwa Serikali inatambua mchango wa wauguzi katika kutekeleza majukumu ya afya kwani wanatumia muda mwingi kukaa na wagonjwa na amewaasa waendelee kuwa na kauli nzuri na sura zenye tabasamu kwa wagonjwa ili kuiheshimisha kazi yao.

Aidha Mganga Mkuu Wilaya Dkt. Thomas Mchomvu amesema kwamba haiwezekani kuzungumzia sekta ya afya bila kuwataja wauguzi na kwamba sehemu kubwa ya watumishi wa afya ni wauguzi ambao wana jukumu kubwa la kulinda na kuhakikisha afya za wagonjwa ziko vizuri.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Dkt. Mchomvu akiongea na watumishi wa afya.

Aidha Dkt Mchomvu ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa katika sekta ya afya ambapo mpaka mwaka 2024, Wilaya ya Kongwa ina vituo vya afya tisa vinavyofanya kazi na kutoa huduma za afya ikiwemo Afya ya uzazi na dharura na kueleza kwamba huo ni utekelezaji mzuri wa ilani ya chama tawala kwa wananchi wake.

Nae Muuguzi Mkuu wa Wilaya Ndg. Cleopa katika risala yake amesema dhumuni la kuadhimisha siku ya wauguzi Duniani ni ili kuimarisha afya ya jamii na kulaani na kupinga vikali vitendo vya wauguzi wasio waaminifu na waadilifu katika kazi zao.

Pia Cleopa ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuruhusu wauguzi kujiendeleza kimasomo, jambo linalowaongezwa wigo mpana wa elimu pamoja na taaluma yao. Ndg. Cleopa pia ameishukuru serikali kwa kuendelea kutoa huduma ya afya ya uzazi na mtoto kwa 88% na kutoa huduma za kujifungua kwa 99% hata katika mazingira magumu na yenye changamoto.

Maadhimisho hayo yaliyokuwa na kaulimbiu "Wauguzi nguvu ya mabadiliko Duniani" wauguzi hao walipata nafasi ya kula kiapo cha maadili chini ya sheria ya wauguzi na wakunga ya Mwaka 2010 mbele ya Mwanasheria Renalda Mkangala wa mahakama ya hakimu makazi mamlaka ya mji mdogo Kibaigwa.

Matangazo

  • Tangazo la nafasi ya kazi June 13, 2025
  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI WALA KIAPO.

    August 04, 2025
  • DED KONGWA AKABIDHI TAA 390 KWA WATUMISHI WA AFYA

    July 28, 2025
  • ECOKAZI WATOA MAFUNZO KUHUSU BIASHARA YA KABONI

    July 24, 2025
  • WASIMAMIZI WA AFYA WANOLEWA UDHIBITI NA UTENGANISHAJI TAZIHA.

    July 23, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.