• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Waziri amtunuku Afisa ugani kwa utendaji makini

Imewekwa: August 17th, 2021

Na Stephen Jackson, Kongwa.

  Waziri wa Kilimo, Prof. Adolf  Faustine Mkenda (Mb) amemtunuku afisa ugani wa kata ya Nghumbi wilayani Kongwa ndugu Charles Mujule , Zawadi ya seti ya Runinga ikiwa ni utekelezaji wa Ahadi aliyoitoa mwezi Mei mwaka 2021, alipotembelea shamba la mtama lenye ukubwa wa Ekari Moja, lililolimwa kitaalamu kwa hisani ya shirika la chakula Duniani ‘’WFP’’ na kusimamiwa na afisa ugani huyo.

  Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Kongwa tarehe 17 Agosti, 2021 mchana ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe, Remidius Mwema Emmanuel ambapo Mhe. Waziri alizungumza na maafisa ugani wa Kata mbalimbali za Wilaya pamoja na wakuu wa Idara. 

  Katika hotuba yake, Mhe. Waziri amewaeleza maafisa ugani kuwa Serikali itawezesha utekelezaji wa majukumu yao kwa kuwapatia vitendea kazi mbalimbali kama vile pikipiki, simu na pembejeo za kilimo ili kuwawezesha kuinua kipato chao ili nao wasaidie kuwainua wakulima.

  Ameongeza kuwa, Serikali inatambua jitihada za maafisa ugani katika kufanikisha mikakati ya Wizara ya Kilimo, hivyo itaendelea kuwathamini, kuwaheshimu na kuwalea ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kikamilifu ikiwa ni pamoja na kutowapangia shughuli tofauti na taaluma zao.

  Kwa upande wake ndugu Mujule amemshukuru mhe. Waziri Prof. Adolf Mkenda kwa kuthamini jitihada zake kiutendaji, na kuwaasa watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi ili kazi wanazozifanya ziwatambulishe.

  Akizunguza baada ya kikao hicho, Mkuu wa Idara ya Kilimo, Wilaya ya Kongwa Ndugu Jackson G. Shija, licha ya kumpongeza bwana Cherles Mujule, pia ameeleza kuwa Wilaya inaendelea na jitihada za kuendeleza mazao ya kimkakati ambayo ni  mtama, Korosho, Alizeti, na Zabibu ambapo kwa mwaka 2020/2021 wilaya imezalisha ziada ya tani 117,978 kwa mazao ya nafaka. Na pia kupitia kikundi cha ZOSEM, Jumla ya tani 18 za mbegu bora ya Alizeti aina ya ''Record'' kwa daraja la kuthibitishwa ubora imezalishwa kwa msimu wa 2020/2021.

  Ziara hiyo ya waziri wa kilimo, ilisindikizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka na Mkutano wake kuhudhuriwa Mkuu wa wilaya ya Kongwa na viongozi mbalimbali wa Halmashauri akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. White Zuberi Mwanzalila, Mkuu wa Idara ya Kilimo ndugu Jackson G. Shija, Diwani wa Kata ya Nghumbi, na Wakuu wa Idara.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.