• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

WENYEVITI WAWILI SERIKALI ZA MITAA WASIMAMISHWA KAZI.

Imewekwa: February 11th, 2025

Mwenyekiti wa Kijiji cha Mlanje Bwana Elisha Mpanda Pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji cha Matongoro, Bw. Joab Chida vilivyopo katika Kata ya Matongoro wilayani Kongwa, wamesimamishwa kazi kutokana na tuhuma za kushindwa kuwajibika na kusababisha migogoro ya ardhi.

Hali hiyo imefikiwa baada ya Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Mayeka Simon Mayeka kutembelea Kata hiyo ili kutatua mgogoro wa mpaka kwa wananchi wa vijiji vya Matongoro na Mlanje ambapo wananchi hao wamewalalamikia wenyeviti hao kuvuruga alama za mipaka ya vijiji hivyo kwa maslahi yao binafsi.

Kufuatia hali hiyo Mh Mayeka amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kuhakikisha anatumia taratibu za kisheria kuwasimamisha kazi wenyeviti hao na kushirikiana na mwanasheria wa Halmashauri kusimamia zoezi la upatikanaji wa wenyeviti wa muda katika vijiji hivyo mpaka pale Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) itakapokamilisha uchunguzi wa tuhuma hizo.

Wakiongea mbele ya Mkuu wa Wilaya, wananchi wa vijiji hivyo wamesema kuwa wenyeviti hao wamekuwa wakishirikiana kuvuruga mipaka inayogawa vijiji hivyo kwa kuuza maeneo ya mbuga ya malisho kwa wakulima, suala ambalo ni kinyume na utaratibu, pia wameongeza kuwa wamekuwa wakitishiwa Maisha pindi wanapojaribu kuhoji kwa viongozi hao.

Aidha, wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Matongoro wameongeza kuwa Mwenyekiti wa kijiji hicho amekuwa akikwamisha shughuli za Serikali na pia wamedai kuwa amekuwa akiongoza Kijiji Kwa mabavu na kudai kuwa hakuna kiongozi wa juu zaidi yake hivyo wanatakiwa kumsikiliza yeye na si mtu mwingine.

Wameongeza kuwa uuzaji wa maeneo hayo kinyume cha taratibu ni utekelezaji wake wa ahadi zake za kilaghai alizozitoa wakati wa kampeni kuwa akichaguliwa atawapatia wakulima maeneo pamoja na ahadi nyinginezo ikiwemo kuingiza kaya maskini katika mfuko wa Tasaf ambapo mpaka sasa inasemekana ameshachukua kiasi cha shilingi milioni tatu na kuuza eneo la malisho lenye hekari 80 kwa wakulima.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kijiji Cha Matongoro Bi. Rosemary Lubengo amekiri kutowajibika kwa Mwenyekiti wa Kijiji hicho na kukwamisha utekelezaji wa maagizo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na utekelezaji wa ilani ya chama cha Mapinduzi kwa maslahi yake binafsi bila kuangalia hali za wananchi ambao alipaswa kuwatumikia.

Nae Afisa ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Bwana Hansi amesema kuwa mipaka iko wazi kwani upimaji wa mipaka ya vijiji vya Matongoro na Mlanje ulifanyika tangu mwaka 2007 na eneo la malisho lilikuwa sehemu ya Kijiji cha Matongoro lakini baada ya Mwenyekiti huyo kuingia madrakani Oktoba mwaka jana akaanza kuuza eneo hilo kwa wakulima na kusema eneo hilo lipo ndani ya Kijiji cha Mlanje na Sio Matongoro hali iliyoibua mgogoro mkubwa kati ya vijiji hivyo vya Mlanje na Matongoro.

Akifunga hotuba yake Mhe. Mayeka amesema kuwa katika suala la migogoro ya ardhi mara kadhaa viongozi wa vijiji wasio waadilifu wamekuwa ni changamoto na kubainisha kuwa eneo la mbuga ni kwaajili ya malisho na sio matumizi mwengine kama kilimo. DC Mayeka pia ametoa rai kwa viongozi wa vijiji kushikamana katika kuyalinda na kusimamia maeneo hayo ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.