• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

Yaliyojiri Mkutano wa Baraza la Madiwani Kongwa Changamoto za Afya na Elimu Zatawala

Imewekwa: May 25th, 2018

Katika Mkutano wa Baraza la Madiwani Wilaya ya Kongwa, Changamoto ya Huduma za Jamii zikiwemo huduma za Afya na Elimu zimechukua nafasi kubwa ya mjadala katika Mkutano wa Robo ya tatu Mwaka wa Fedha 2017/18 kilichofanyika Katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa tarehe 24-05-2018.

Madiwani wa Kata ya Iduo, Songambele, Chitego na Pandambili walielezea changamoto za Huduma ya Afya zinazofanana ikiwemo kukosekana kwa dawa muhimu zikiwemo Paracetamol, mipira ya kuvaa mikononi (Gloves) kwa ajili ya kuhudumia akina mama wakati wa Uzazi Katika vituo vya Afya na Zahanati.

Changamoto nyingine kubwa iliyojadiliwa ni upungufu wa Walimu na Wahudumu wa Afya kwani kuwepo kwa mhudumu mmoja-mmoja katika vituo vingi vya Afya ni hali inayodhoofisha huduma za Afya na hupelekea wakati mwingine huduma kukosekana, mtumishi huyo anapopata likizo, dharula za kikazi au kuugua.

Aidha, Diwani wa Kata ya Mlali Mhe Richard Mngurumi alisema Zahanati ya Kijiji cha Ihanda imefungwa kutokana na watumishi walio kuwepo; mmoja aliondolewa kwa vyeti vya kugushi na mwingine aliomba uhamisho kama haki yake. Hivyo, anaiomba Serikali kuisaidia Kata hiyo kwa kupeleka mhudumu katika kituo hicho cha ili kuwasaidia wananchi wa kijiji hicho kutatua matatizo yao ya kiafya.

Mwenyekiti wa kamati ya Huduma za Jamii Diwani wa Kata ya Msunjulile Mhe. Chilingo Chimeledya amekiri kuwepo kwa Zahanati ambazo hazijafunguliwa na ameliambia Baraza Zahanati hizohazijafunguliwa kutokana na sababu ambalo zipo nje ya uwezo kutokana na Kutokuwa na wahudumu wa kuhudumia katika Zahanati hizo.

Hivyo, katika Zahanati ya Ihanda Halmashauri kupitia Idara ya Afya itafanya utaratibu mhudumu apatikane ili ifunguliwe; Pia, Serikali itakapoajiri kutakuwa na kipaumbele kwa Zahanati, vituo vya Afya na Shule zenye upungufu wa walimu.

Aidha, kufuatia changamoto za elimu wilayani Kongwa ikiwemo upungufu wa Madarasa na Vyoo, Baraza limeridhia hoja ya uanzishwaji wa Mfuko wa Elimu wa Wilaya ambao utakusanya fedha na kuwekwa katika akaunti za Kata.

Akiwasilisha Taarifa ya Kamati katika Mkutano wa Baraza la Madiwani Mhe. Chimeledya alisema, Mwenyekiti wa Kamati za Huduma za Jamii ameeleza kwamba Kamati ilishauri kila mwananchi mwenye umri wa miaka 18 atapaswa kuchangia TShs.10,000/= kwa mwaka ambapo fedha hizo zitatumika kutatua Changamoto za kielimu Katika kila Kata.

Kadhalika, Kamati ya Huduma za Jamii ilishauri viongozi wa Kata watumike kuhamasisha na kuhimiza wananchi kutoa michango hiyo, pia viandaliwe vitabu vya stakadhi za malipo, wakabidhiwe watendaji Vijiji na Kata vikiambatana na onyo kali juu ya ubadhilifu wowote utakajitokeza.

Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Kibaigwa Mhe. Samweli Mganga ameiomba Serikali kuhakikisha inafanya usajili kwa shule za mkondo zilizotimiza vigezo ili kuondoa adha ya umbali wa shule kwa  wanafunzi na kuwangezea ari ya Kusoma.

Pia, Diwani wa Kata ya Hogoro Mhe. Drank Mgata ameitaka Halmashauri hiyo kupeleka mwalimu wa Kike Katika Shule ya msingi Mkutani kwani kuna walimu wa kiume tupu ili kuwasaidia wanafunzi wa kike wanaopevuka ambapo kuelekezwa na walimu wa kiume ni kinyume na mila na desturi za kiafrika.

Sambamba na Changamoto hizo kuchukua nafasi kubwa Katika mjadala Kikao hicho kilijadili mambo Mbalimbali yakiwemo ya kiuchumi, Mazingira, na udhibiti wa maambukizi ya Ukimwi ambapo Mwenyekiti wa Kamati ya Kudhibiti maambukizi ya UKIMWI Diwani wa Kata Ya Mkoka Richard Mwite amewataka Madiwani kuhamasisha wananchi upimaji wa VVU Hiari.


Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.