• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kongwa District Council
Kongwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Idara ya Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi & Zima moto
      • Mazingira na Usafi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Madini
    • Biashara
    • Viwanda
    • Mawasiliano
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Ardhi
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma za TEHAMA
    • Usimamizi & Ufuatiliaji wa Miradi
    • Huduma za Ushauri na Ufundi
    • Ruzuku ya Kunusuru Kaya Masikini
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Inayoendela
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
    • Miradi iliyokamilika
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo
      • Utawala
      • Maendeleo ya Jamii
      • Nishati
  • Machapisho
    • Sheria ndogo ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati wa Halmashauri
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Majarida
    • Gazeti la Serikali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video za Shughuli za Maendeleo
  • Michezo
    • Michezo
    • Sanaa

ZIARA YA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA MHE. WASIRA WILAYANI KONGWA.

Imewekwa: April 25th, 2025

Makamu mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Stephen Wasira amewaasa wauguzi kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha wanatoa huduma nzuri na kuzingatia utu ili kuhakikisha uboreshaji mkubwa wa miundombinu uliofanywa na Serikali ya awamu ya sita, unaleta tija kwa wananchi. 

Mhe. Wasira ameyasema hayo alipotembelea Wilaya ya Kongwa ambapo amefanya ukaguzi wa jengo la wodi ya Wazazi katika hospitali ya Wilaya, pamoja na ujenzi wa jengo jipya la Halmashauri na kupata wasaa wa kuongea na wananchi wa Wilaya ya Kongwa katika mkutano wa hadhara.

Akisoma taarifa mbele ya Makamu Mwenyekiti kabla ya kukagua wodi ya wazazi, dkt. Thomas Mchomvu ameeleza kuwa jengo linahudumia wazazi waliotoka kujifungua, ikiwemo waliotoka kufanyiwa upasuaji ambao wanakuwa wanaendelea kupatiwa huduma, na kuongeza kuwa jengo pia lina sehemu maalum kwa ajili ya watoto wachanga wanaozaliwa kabla ya muda wao.

Aidha dtk. Mchomvu ameeleza kuwa ongezeko la upatikanaji wa bidhaa za afya hospitalini limepunguza kwa kiasi kikubwa malalamiko ya ukosefu wa bidhaa za afya na kusaidia wananchi kupata huduma hizo wanapozihitaji.

Vilevile dkt. Thomas Mchomvu ameainisha kuwa toka jengo lianze kutumika mwaka 2023, idadi ya wazazi 1097 wamepata watoto katika jengo hilo na kuongeza kuwa watoto waliozaliwa kabla ya muda wao ambao wamekuwa wakipatiwa rufaa wamekuwa wakihudumiwa kweye jengo hilo.

Aidha, Mhe. Wasira wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara, amegusia baadhi ya mafanikio katika Wilaya ya Kongwa na kueleza kuwa Serikali imefanikiwa kujenga vituo vya afya 5, zahanati 12, upatikanaji wa Maji 88%, umeme katika Vijiji vyote 87 na vitongoji 175 kati ya 176 na kuongeza kuwa katika Ilani ijayo ya Chama cha Mapinduzi, kipaumbele kimewekwa katika kukuza uchumi na kubadili maisha ya watu kwa kuweka matrekta na kukodisha kwa wakulima ili kuchochea kilimo cha umwagiliaji na ujenzi wa nyumba nzuri za wananchi.

Ziara ya makamu mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mhe. Stephen Wasira katika Wilaya ya Kongwa ni muendelezo wa ziara yake ya kikazi kutembelea Halmashauri na Wilaya zote za Mkoa wa Dodoma kujionea mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita na kupima utakelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi katika vipaumbele mbalimbali vinavyolenga kuwaletea wananchi maendeleo.

Matangazo

  • Majina ya mipaka ya vijiji na vitongoji vilivyopo katika eneo la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa. October 16, 2024
  • TANGAZO LA MAELEKEZO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024. October 16, 2024
  • Tangazo la nafasi za ajira za mkataba October 07, 2024
  • Tangazo la kufunguliwa kwa dirisha la utoaji mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu- Oktoba 1 2024 October 02, 2024
  • Tazama Yote

Habari Mpya

  • MGOGORO WA MPAKA CHIGWINGWILI - HOGORO KUTAFUTIWA UFUMBUZI.

    May 08, 2025
  • VIKUNDI VYASISITIZWA KUWA NA USHIRIKIANO MZURI NA VIONGOZI PAMOJA NA WATAALAM

    May 05, 2025
  • VIKUNDI 21 VYAKABIDHIWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YA HALMASHAURI

    April 28, 2025
  • DC MAYEKA AKABIDHI MISAADA

    April 27, 2025
  • Tazama Yote

Video

zoezi la uandikishwaji daftari la Mpiga Kura kuanza 11-20 Oktoba, 2024
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Mbalmbali
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Miongozo
  • Miradi iliyokamilika
  • Miradi inayoendelea
  • Taarifa kwa Umma
  • Zabuni
  • Kituo cha Biashara (OSBC) Kongwa
  • Orodha ya Madiwani na Mawasiliano

Viunganishi Linganifu

  • Time huru ya Uchaguzi
  • Tovuti ya Taifa
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala ya Serikali Mtandao (e-GA)

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Rekodi ya Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya

    Anuani ya Posta: S.L.P 57 Kongwa, Dodoma

    Simu ya Mezani: +255 26 2370031

    Simu ya Mkononi: +255 713399349

    Barua pepe : ded@kongwadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti
    • Tahadhari kwenye Barua pepe

Copyright ©2022 Kongwa District Council . All rights reserved.